< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Célébrez l'Éternel, car il est bon, car sa miséricorde demeure à toujours!
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Qu'ainsi disent les rachetés de l'Éternel, ceux qu'il a rachetés de la main de l'oppresseur,
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Et qu'il a rassemblés des pays d'orient et d'occident, de l'aquilon et du midi.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Ils erraient par le désert, dans un chemin solitaire; ils ne trouvaient point de ville habitable.
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Ils étaient affamés et altérés; leur âme défaillait en eux.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
Il les a conduits par le droit chemin, pour arriver à une ville habitable.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
Car il a rassasié l'âme altérée, et rempli de biens l'âme affamée.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Ceux qui habitaient les ténèbres et l'ombre de la mort, retenus dans l'affliction et dans les fers,
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
Pour avoir été rebelles aux paroles de Dieu, et avoir méprisé le conseil du Très-Haut;
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Il avait humilié leur cœur par la souffrance; ils succombaient loin de tout secours.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
Il les a tirés des ténèbres et de l'ombre de la mort; il a rompu leurs liens.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Car il a brisé les portes d'airain, et rompu les barreaux de fer.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Les insensés qui étaient affligés à cause de la voie de leurs trangressions et de leurs iniquités;
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Leur âme avait en horreur toute nourriture; ils touchaient aux portes de la mort.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse; et il les a délivrés de leurs angoisses.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Il a envoyé sa parole, et il les a guéris, et les a retirés de leurs tombeaux.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Qu'ils célèbrent l'Éternel pour sa bonté, pour ses merveilles envers les fils des hommes!
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Qu'ils offrent des sacrifices d'actions de grâces, et racontent ses œuvres en chantant de joie!
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Ceux qui descendent sur la mer dans des navires, et qui trafiquent sur les grandes eaux,
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
Ceux-là ont vu les œuvres de l'Éternel, et ses merveilles dans les lieux profonds.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
Il parla, et fit lever un vent de tempête, qui souleva les vagues de la mer.
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
Ils montent aux cieux; ils descendent aux abîmes; leur âme se fond d'angoisse.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
Ils tournoient et chancellent comme un homme ivre; toute leur sagesse leur manque.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Alors ils ont crié à l'Éternel dans leur détresse, et il les a retirés de leurs angoisses.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Il arrête la tempête, la changeant en calme, et les ondes se taisent.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
Ils se réjouissent de ce qu'elles sont calmées; et il les conduit au port qu'ils désiraient.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Qu'ils célèbrent la bonté de l'Éternel, et ses merveilles envers les fils des hommes!
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Qu'ils l'exaltent dans l'assemblée du peuple; qu'ils le louent dans le conseil des anciens!
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Il change les fleuves en désert, et les sources d'eaux en un sol aride;
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
La terre fertile en lande salée, à cause de la méchanceté de ses habitants.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Il change le désert en étang, et la terre aride en sources d'eaux.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
Il y fait habiter ceux qui étaient affamés; et ils fondent une ville pour l'habiter.
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
Ils ensemencent des champs et plantent des vignes, qui rendent du fruit tous les ans.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Il les bénit, et ils se multiplient extrêmement; il ne laisse point diminuer leur bétail.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Puis, ils sont amoindris et humiliés par l'oppression, le malheur et la souffrance.
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
Il répand le mépris sur les grands, et les fait errer dans un désert sans chemin.
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
Mais il relève le pauvre de l'affliction, et rend les familles nombreuses comme des troupeaux.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Les hommes droits le voient et s'en réjouissent; mais tous les injustes ont la bouche fermée.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Que celui qui est sage prenne garde à ces choses, et considère les bontés de l'Éternel.