< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
to give thanks to/for LORD for be pleasing for to/for forever: enduring kindness his
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
to say to redeem: redeem LORD which to redeem: redeem them from hand enemy
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
and from land: country/planet to gather them from east and from west from north and from sea
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
to go astray in/on/with wilderness in/on/with wilderness way: journey city seat not to find
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
hungry also thirsty soul their in/on/with them to enfeeble
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
and to cry to(wards) LORD in/on/with distress to/for them from distress their to rescue them
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
and to tread them in/on/with way: road upright to/for to go: went to(wards) city seat
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
to give thanks to/for LORD kindness his and to wonder his to/for son: child man
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
for to satisfy soul to rush and soul hungry to fill good
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
to dwell darkness and shadow prisoner affliction and iron
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
for to rebel word God and counsel Most High to spurn
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
and be humble in/on/with trouble heart their to stumble and nothing to help
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
and to cry out to(wards) LORD in/on/with distress to/for them from distress their to save them
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
to come out: send them from darkness and shadow and bond their to tear
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
to give thanks to/for LORD kindness his and to wonder his to/for son: child man
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
for to break door bronze and bar iron to cut down/off
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
fool(ish) from way: journey transgression their and from iniquity: crime their to afflict
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
all food to abhor soul: myself their and to touch till gate death
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
and to cry out to(wards) LORD in/on/with distress to/for them from distress their to save them
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
to send: depart word his and to heal them and to escape (from pit their *LAH(b)*)
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
to give thanks to/for LORD kindness his and to wonder his to/for son: child (man *LAH(b)*)
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
and to sacrifice sacrifice thanksgiving and to recount deed: work his (in/on/with cry *L(abh)*)
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
to go down [the] sea in/on/with fleet to make: do work in/on/with water (many *L(abh)*)
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
they(masc.) to see: see deed: work LORD and to wonder his (in/on/with depth *L(abh)*)
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
and to say and to stand: rise spirit: breath tempest and to exalt (heap: wave his *L(abh)*)
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
to ascend: copulate heaven to go down abyss soul: myself their in/on/with distress: harm (to melt *LB(ah)*)
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
to celebrate and to shake like/as drunken and all wisdom their (to swallow up *LB(ah)*)
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
and to cry to(wards) LORD in/on/with distress to/for them and from distress their to come out: send them
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
to arise: establish tempest to/for silence and be silent heap: wave their
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
and to rejoice for be quiet and to lead them to(wards) haven pleasure their
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
to give thanks to/for LORD kindness his and to wonder his to/for son: child man
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
and to exalt him in/on/with assembly people and in/on/with seat old: elder to boast: praise him
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
to set: make river to/for wilderness and exit water to/for parched
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
land: country/planet fruit to/for saltiness from distress: evil to dwell in/on/with her
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
to set: put wilderness to/for pool water and land: country/planet dryness to/for exit water
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
and to dwell there hungry and to establish: make city seat
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
and to sow land: country and to plant vineyard and to make: do fruit produce
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
and to bless them and to multiply much and animal their not to diminish
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
and to diminish and to bow from coercion distress: evil (and sorrow *L(abh)*)
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
to pour: pour contempt upon noble and to go astray them in/on/with formlessness not way: road
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
and to exalt needy from affliction and to set: make like/as flock family
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
to see: see upright and to rejoice and all injustice to gather lip her
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
who? wise and to keep: careful these and to understand kindness LORD