< Zaburi 106 >
1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Aleluja! Slavite Gospoda, ker je dober, ker je vekomaj milost njegova.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Kdo bi dopovedal najvišjo moč Gospodovo, oznanil vso hvalo njegovo?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
O blagor jim, ki se držé postave té, ki delajo pravico vsak čas!
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Spomni se me, Gospod, po blagovoljnosti, katero izkazuješ svojemu ljudstvu, obišči me z blaginjo svojo.
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
Da uživam izvoljenih tvojih dobroto, da se radujem radosti naroda tvojega; da se s posestjo tvojo ponašam.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
Grešili smo z očeti svojimi: krivično smo delali, ravnali hudobno.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Očetje naši niso umeli v Egiptu čudovitih dél tvojih; spominjali se niso milosti tvojih obilosti; temuč priliko so dajali izpremeniti jih pri morji, ko so stopali v morje trstovito.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Vendar jih je rešil zavoljo imena svojega, da bi pokazal svojo moč.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
Ker zarotil je trstovito morje, in posušilo se je; in peljal jih je skozi valove kakor skozi puščavo.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
Tako jih je rešil roke sovražnikove; otel jih je neprijateljeve roke.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
Pokrile pa so vode njih sovražnike; eden izmed njih ni ostal.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Da sì so verjeli besedam njegovim, peli hvalo njegovo,
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
Pozabili so naglo dél njegovih; čakali niso sveta njegovega.
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
Ampak iz poželjivosti v puščavi izkušali so Boga mogočnega v samoti.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
Tako da je podelivši jim, kar so prosili, poslal kugo nad nje.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
Potem ko so bili nevoščljivi Mojzesu v šatorji, Aronu svetniku Gospodovemu,
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
Odprla se je zemlja in požrla Datana in zagrnila je drhal Abiramovo.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
In vnel se je ogenj v njih drhal, in s plamenom požgal krivične.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
Naredili so tele na Horebu, in klanjali so se podobi.
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
In premenivši čast svojo v podobo vola, ki travo jé,
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
Pozabili so Boga mogočnega, rešitelja svojega, kateri je bil storil velike reči v Egiptu,
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
Čudovita dela v deželi Kamovi, strašna pri trstovitem morji.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
Zatorej je rekel, da jih bode pogubil; ko bi ne bil Mojzes, izvoljenec njegov, stopil v ón predór pred njim, da bi odvrnil jezo njegovo, da jih ne pogubi.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
Zavrgli so tudi zaželeno deželo, ne verujoč besedi njegovi.
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
In godrnjaje v šatorih svojih niso poslušali glasú Gospodovega.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
Zatorej je dvignil roko svojo ter prisegel, da jih podere v sami puščavi.
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
In da podere seme njih med narodi, in razkropi jih po deželah.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
Razen tega so se združili tudi z malikom Peorjem, in jedli mrtvih daritve.
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
Klicali so tako Boga v nevoljo z deli svojimi, da je pridrla nad nje nadloga.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Dokler ni vstal Pineas in storil sodbo, ter je bila ustavljena tista nadloga;
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
Kar se mu je štelo za pravico, od roda do roda vekomaj.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
Enako so razdražili gorečo jezo pri vodah prepira, tako da se je slabo godilo Mojzesu zavoljo njih.
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
Ko so bili razdražili duha njegovega, in je izgovoril z ustnami svojimi razdraženje svoje:
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
Pokončali niso onih ljudstev, za katera jim je bil zapovedal Gospod;
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
Ampak pomešali so se z onimi narodi in naučili se njih dél.
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
In čestili so njih podobe, katere so bile njim v izpotiko.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
Ker darovali so sinove svoje in hčere svoje hudobnim duhovom;
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
In prelivali so nedolžno kri, kri sinov svojih in hčer svojih, katere so darovali podobam Kanaanskim, tako da je bila zemlja onečiščena z njih moritvami.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
In oskrunjali so se sè svojimi deli; prešestvovali z dejanji svojimi.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
Zatorej se je razsrdil Gospod nad ljudstvom svojim in studil svojo posest,
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
Tako da jih je dal v roko narodom, da bi jim gospodovali njih sovražniki, črtilci,
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
In jih zatirali njih neprijatelji, in da bi se poniževali pod njih roko.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Mnogokrat jih je rešil, dasì so ga bili razsrdili z naklepom svojim, in so bili ponižani zavoljo krivice svoje.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
Ozrl se je na njih stisko, slišal je njih vpitje.
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
In spomnivši se zá nje zaveze svoje, kesal se je po obilosti milosti svojih;
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
Tako da jim je izkazal usmiljenje pred vsemí, kateri so jih v sužnjosti imeli.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Reši nas, Gospod, Bog naš, in zberi nas izmed tistih narodov, da slavimo sveto ime tvoje, in se s hvaljenjem priporočamo v hvali tvoji,
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Blagoslovljen Gospod, Izraelov Bog, od veka do veka in vse ljudstvo naj govori: Aleluja!