< Zaburi 106 >
1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
ALLELUIA. Celebrate il Signore; perciocchè [egli è] buono; Perciocchè la sua benignità [è] in eterno.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Chi potrà raccontar le potenze del Signore? [Chi] potrà pubblicar tutta la sua lode?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Beati coloro che osservano la dirittura, Che fanno ciò ch'è giusto in ogni tempo.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Ricordati di me, o Signore, Secondo la [tua] benevolenza verso il tuo popolo; Visitami colla tua salute;
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
Acciocchè io vegga il bene de' tuoi eletti, [E] mi rallegri dell'allegrezza della tua gente, [E] mi glorii colla tua eredità.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
Noi, e i nostri padri, abbiam peccato, Abbiamo operato iniquamente ed empiamente.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
I nostri padri in Egitto non considerarono le tue maraviglie, Non si ricordarono della grandezza delle tue benignità; E si ribellarono presso al mare, nel Mar rosso.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Ma pure [il Signore] li salvò per l'amor del suo Nome, Per far nota la sua potenza;
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
E sgridò il Mar rosso, ed esso si seccò; E li fece camminar per gli abissi, come [per] un deserto.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
E li salvò di man di coloro che li odiavano, E li riscosse di man del nemico.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
E le acque copersero i lor nemici; E non ne scampò pure uno
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Allora credettero alle sue parole; Cantarono la sua lode.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
[Ma] presto dimenticarono le sue opere; Non aspettarono il suo consiglio;
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
E si accessero di cupidigia nel deserto; E tentarono Iddio nella solitudine.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
Ed egli diede loro ciò che chiedevano; Ma mandò la magrezza nelle lor persone.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
Oltre a ciò furono mossi d'invidia contro a Mosè, nel campo; [E] contro ad Aaronne, il Santo del Signore.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
La terra si aperse, e tranghiottì Datan, E coperse il seguito di Abiram.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
E il fuoco arse la lor raunanza; La fiamma divampò gli empi.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
Fecero un vitello in Horeb, E adorarono una statua di getto;
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
E mutarono la lor gloria In una somiglianza di bue che mangia l'erba.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
Dimenticarono Iddio, lor Salvatore, Il quale aveva fatte cose grandi in Egitto;
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
Cose maravigliose nel paese di Cam, Tremende al Mar rosso.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
Onde egli disse di sterminarli; Se non che Mosè, suo eletto, si presentò alla rottura davanti a lui, Per istornar l'ira sua che non distruggesse.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
Disdegnarono ancora il paese desiderabile; Non credettero alla sua parola.
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
E mormorarono ne' lor tabernacoli; Non attesero alla voce del Signore.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
Onde egli alzò loro la mano, Che li farebbe cader nel deserto;
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
E che farebbe cader la lor progenie fra le genti, E che li dispergerebbe per li paesi.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
Oltre a ciò si congiunsero con Baal-peor, E mangiarono de' sacrificii de' morti;
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
E dispettarono [Iddio] co' lor fatti, Onde la piaga si avventò a loro.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Ma Finees si feve avanti, e fece giudicio; E la piaga fu arrestata.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
E ciò gli fu reputato per giustizia, Per ogni età, in perpetuo.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
Provocarono ancora [il Signore] ad ira presso alla acque di Meriba, Ed avvenne del male a Mosè per loro.
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
Perciocchè inasprirono il suo spirito; Onde egli parlò disavvedutamente colle sue labbra.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
Essi non distrussero i popoli, Che il Signore aveva lor detto;
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
Anzi si mescolarono fra le genti, Ed impararono le loro opere;
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
E servirono a' loro idoli, E quelli furono loro per laccio;
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
E sacrificarono i lor figluoli. E le lor figliuole a' demoni;
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
E sparsero il sangue innocente, Il sangue de' lor figliuoli e delle lor figliuole, I quali sacrificarono agl'idoli di Canaan; E il paese fu contaminato di sangue.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
Ed essi si contaminarono per le loro opere, E fornicarono per li lor fatti.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
Onde l'ira del Signore si accese contro al suo popolo, Ed egli abbominò la sua eredità;
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
E li diede in man delle genti; E quelli che li odiavano signoreggiarono sopra loro.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
E i lor nemici li oppressarono; Ed essi furono abbassati sotto alla lor mano.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Egli li riscosse molte volte; Ma essi lo dispettarono co' lor consigli, Onde furono abbattuti per la loro iniquità.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
E pure egli ha riguardato, quando [sono stati] in distretta; Quando ha udito il lor grido;
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
E si è ricordato inverso loro del suo patto, E si è pentito, secondo la grandezza delle sue benignità.
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
Ed ha renduti loro pietosi Tutti quelli che li avevano menati in cattività.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Salvaci, o Signore Iddio nostro, E raccoglici d'infra le genti; Acciocchè celebriamo il Nome della tua santità, [E] ci gloriamo nella tua lode.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Benedetto [sia] il Signore Iddio d'Israele di secolo in secolo. Or dica tutto il popolo: Amen. Alleluia.