< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
הללויה הודו ליהוה כי טוב כי לעולם חסדו׃
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
מי ימלל גבורות יהוה ישמיע כל תהלתו׃
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
אשרי שמרי משפט עשה צדקה בכל עת׃
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
זכרני יהוה ברצון עמך פקדני בישועתך׃
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
לראות בטובת בחיריך לשמח בשמחת גויך להתהלל עם נחלתך׃
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
חטאנו עם אבותינו העוינו הרשענו׃
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
אבותינו במצרים לא השכילו נפלאותיך לא זכרו את רב חסדיך וימרו על ים בים סוף׃
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
ויושיעם למען שמו להודיע את גבורתו׃
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
ויגער בים סוף ויחרב ויוליכם בתהמות כמדבר׃
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
ויושיעם מיד שונא ויגאלם מיד אויב׃
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
ויכסו מים צריהם אחד מהם לא נותר׃
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
ויאמינו בדבריו ישירו תהלתו׃
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
מהרו שכחו מעשיו לא חכו לעצתו׃
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
ויתאוו תאוה במדבר וינסו אל בישימון׃
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
ויתן להם שאלתם וישלח רזון בנפשם׃
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
ויקנאו למשה במחנה לאהרן קדוש יהוה׃
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
תפתח ארץ ותבלע דתן ותכס על עדת אבירם׃
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
ותבער אש בעדתם להבה תלהט רשעים׃
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
יעשו עגל בחרב וישתחוו למסכה׃
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
וימירו את כבודם בתבנית שור אכל עשב׃
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
שכחו אל מושיעם עשה גדלות במצרים׃
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
נפלאות בארץ חם נוראות על ים סוף׃
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
ויאמר להשמידם לולי משה בחירו עמד בפרץ לפניו להשיב חמתו מהשחית׃
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
וימאסו בארץ חמדה לא האמינו לדברו׃
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
וירגנו באהליהם לא שמעו בקול יהוה׃
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
וישא ידו להם להפיל אותם במדבר׃
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
ולהפיל זרעם בגוים ולזרותם בארצות׃
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
ויצמדו לבעל פעור ויאכלו זבחי מתים׃
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
ויכעיסו במעלליהם ותפרץ בם מגפה׃
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
ויעמד פינחס ויפלל ותעצר המגפה׃
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
ותחשב לו לצדקה לדר ודר עד עולם׃
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
ויקציפו על מי מריבה וירע למשה בעבורם׃
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
כי המרו את רוחו ויבטא בשפתיו׃
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
לא השמידו את העמים אשר אמר יהוה להם׃
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
ויתערבו בגוים וילמדו מעשיהם׃
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
ויעבדו את עצביהם ויהיו להם למוקש׃
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
ויזבחו את בניהם ואת בנותיהם לשדים׃
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
וישפכו דם נקי דם בניהם ובנותיהם אשר זבחו לעצבי כנען ותחנף הארץ בדמים׃
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
ויטמאו במעשיהם ויזנו במעלליהם׃
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
ויחר אף יהוה בעמו ויתעב את נחלתו׃
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
ויתנם ביד גוים וימשלו בהם שנאיהם׃
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
וילחצום אויביהם ויכנעו תחת ידם׃
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
פעמים רבות יצילם והמה ימרו בעצתם וימכו בעונם׃
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
וירא בצר להם בשמעו את רנתם׃
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
ויזכר להם בריתו וינחם כרב חסדו׃
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
ויתן אותם לרחמים לפני כל שוביהם׃
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
הושיענו יהוה אלהינו וקבצנו מן הגוים להדות לשם קדשך להשתבח בתהלתך׃
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
ברוך יהוה אלהי ישראל מן העולם ועד העולם ואמר כל העם אמן הללו יה׃

< Zaburi 106 >