< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Hallelujah! Danket dem HERRN, denn er ist gütig, seine Gnade währt ewiglich!
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Wer kann die Machttaten des HERRN beschreiben und allen seinen Ruhm verkünden?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Wohl denen, die das Recht beachten, die Gerechtigkeit üben allezeit!
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Gedenke meiner, o HERR, aus Gnaden gegen dein Volk, suche mich heim mit deinem Heil,
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
daß ich einen Einblick bekomme in das Wohlergehen deiner Auserwählten, mich freue an der Freude deines Volkes und mich deines Erbteils rühme.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
Wir haben gesündigt samt unsern Vätern, wir haben verkehrt gehandelt, wir haben gefrevelt.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Unsre Väter in Ägypten hatten nicht acht auf deine Wunder, sie gedachten nicht an die Größe deiner Güte und waren widerspenstig am Meer, am Schilfmeer.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Aber er half ihnen um seines Namens willen, um seine Stärke kundzutun.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
Und er bedrohte das Schilfmeer, daß es vertrocknete, und ließ sie durch die Tiefen gehen wie auf einer Steppe.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
Und er rettete sie von der Hand des Hassers und erlöste sie aus der Hand des Feindes.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
Und das Wasser bedeckte ihre Bedränger, nicht einer von ihnen blieb übrig.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Da glaubten sie seinen Worten und sangen sein Lob.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
Aber sie vergaßen seine Werke bald, sie warteten nicht auf seinen Rat,
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
sondern ließen sich gelüsten in der Wüste und versuchten Gott in der Einöde.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
Und er gab ihnen, was sie forderten, sandte aber eine Seuche unter sie.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
Und sie wurden eifersüchtig auf Mose im Lager, auf Aaron, den Heiligen des HERRN.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
Da tat sich die Erde auf und verschlang Datan und bedeckte die Rotte Abirams;
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
und Feuer verzehrte ihre Rotte, die Flamme versengte die Gottlosen.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
Sie machten ein Kalb am Horeb und warfen sich nieder vor dem gegossenen Bild.
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
Sie vertauschten ihre Herrlichkeit gegen das Abbild eines Stiers, der Gras frißt.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
Sie vergaßen Gottes, ihres Retters, der große Dinge in Ägypten getan,
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
Wunder im Lande Hams, Furchtbares am Schilfmeer.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
Und er gedachte sie zu vertilgen, wenn nicht Mose, sein Auserwählter, in den Riß getreten wäre vor seinem Angesicht, um seinen Grimm abzuwenden, daß er sie nicht vertilgte.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
Sie verachteten das liebliche Land, sie glaubten seinem Worte nicht.
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
Und sie murrten in ihren Zelten, sie gehorchten nicht der Stimme des HERRN.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
Da erhob er seine Hand [und schwur], sie niederzustrecken in der Wüste
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
und ihren Samen unter die Nationen zu werfen und sie zu zerstreuen in die Länder.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
Und sie hängten sich an den Baal-Peor und aßen Opfer der toten [Götzen],
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
und sie erzürnten ihn mit ihrem Tun; da brach die Plage unter ihnen aus.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Aber Pinehas trat auf und übte Gericht, so daß die Plage aufgehalten ward.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
Das wurde ihm zur Gerechtigkeit gerechnet auf alle Geschlechter, in Ewigkeit.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
Und sie erzürnten ihn am Haderwasser, und es erging Mose übel um ihretwillen.
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
Denn sie betrübten seinen Geist, und er redete unbedacht mit seinen Lippen.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
Sie vertilgten die Völker nicht, von denen der HERR ihnen gesagt hatte;
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
sondern ließen sich ein mit den Heiden und lernten ihre Weise.
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
Und sie dienten ihren Götzen, und diese wurden ihnen zum Fallstrick.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
Und sie opferten ihre Söhne und ihre Töchter den bösen Geistern.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
Und sie vergossen unschuldiges Blut, das Blut ihrer Söhne und ihrer Töchter, welche sie den Götzen Kanaans opferten, und so wurde das Land durch Blutschulden entweiht.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
Und sie befleckten sich mit ihren Werken und hurten mit ihrem Tun.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
Da entbrannte der Zorn des HERRN wider sein Volk, und er faßte einen Abscheu gegen sein Erbe.
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
Und er gab sie in die Hand der Nationen, daß ihre Hasser über sie herrschten.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
Und ihre Feinde bedrückten sie, und sie wurden gedemütigt unter ihre Hand.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Er errettete sie oftmals; aber sie widerstrebten ihm mit ihren Anschlägen und kamen herunter durch eigene Schuld.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
Aber er sah ihre Not an, als er ihr Schreien hörte,
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
und gedachte seines Bundes mit ihnen und empfand Mitleid nach seiner großen Huld
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
und ließ sie Erbarmen finden bei denen, die sie gefangen hielten.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Hilf uns, HERR, unser Gott, sammle uns aus den Heiden, daß wir deinem heiligen Namen danken und uns glücklich preisen, zu deinem Ruhm!
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Gelobt sei der HERR, der Gott Israels, von Ewigkeit zu Ewigkeit, und alles Volk soll sagen: Amen! Hallelujah!

< Zaburi 106 >