< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alleluya. Kouleche ye to the Lord, for he is good; for his mercy is with outen ende.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Who schal speke the powers of the Lord; schal make knowun alle hise preisyngis?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Blessid ben thei that kepen dom; and doon riytfulnesse in al tyme.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Lord, haue thou mynde on vs in the good plesaunce of thi puple; visite thou vs in thin heelthe.
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
To se in the goodnesse of thi chosun men, to be glad in the gladnes of thi folk; that thou be heried with thin eritage.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
We han synned with oure fadris; we han do vniustli, we han do wickidnesse.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Oure fadris in Egipt vndirstoden not thi merueils; thei weren not myndeful of the multitude of thi merci. And thei stiynge in to the see, in to the reed see, terreden to wraththe;
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
and he sauede hem for his name, that `he schulde make knowun his power.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
And he departide the reed see, and it was dried; and he lede forth hem in the depthis of watris as in deseert.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
And he sauede hem fro the hond of hateris; and he ayen bouyte hem fro the hond of the enemye.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
And the watir hilide men troublynge hem; oon of hem abood not.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
And thei bileueden to hise wordis; and thei preisiden the heriynge of hym.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
Thei hadden `soone do, thei foryaten hise werkis; and thei abididen not his councel.
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
And thei coueitiden coueitise in deseert; and temptiden God in a place with out watir.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
And he yaf to hem the axyng of hem; and he sente fulnesse in to the soulis of hem.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
And thei wraththiden Moyses in the castels; Aaron, the hooli of the Lord.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
The erthe was opened, and swolewid Datan; and hilide on the congregacioun of Abiron.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
And fier brente an hiye in the synagoge of hem; flawme brente synneris.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
And thei maden a calf in Oreb; and worschipiden a yotun ymage.
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
And thei chaungiden her glorie; in to the liknesse of a calf etynge hei.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
Thei foryaten God, that sauede hem, that dide grete werkis in Egipt,
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
merueils in the lond of Cham; feerdful thingis in the reed see.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
And God seide, that he wolde leese hem; if Moises, his chosun man, hadde not stonde in the brekyng of his siyt. That he schulde turne awei his ire; lest he loste hem.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
And thei hadden the desirable lond for nouyt, thei bileueden not to his word, and thei grutchiden in her tabernaclis;
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
thei herden not the vois of the Lord.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
And he reiside his hond on hem; to caste doun hem in desert.
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
And to caste awei her seed in naciouns; and to leese hem in cuntreis.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
And thei maden sacrifice to Belfagor; and thei eeten the sacrificis of deed beestis.
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
And thei wraththiden God in her fyndyngis; and fallyng was multiplied in hem.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
And Fynees stood, and pleeside God; and the veniaunce ceesside.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
And it was arrettid to hym to riytfulnesse; in generacioun and in to generacioun, til in to with outen ende.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
And thei wraththiden God at the watris of ayenseiyng; and Moises was trauelid for hem, for thei maden bittere his spirit,
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
and he departide in his lippis.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
Thei losten not hethen men; whiche the Lord seide to hem.
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
And thei weren meddlid among hethene men, and lerneden the werkis of hem,
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
and serueden the grauen ymagis of hem; and it was maad to hem in to sclaundre.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
And thei offriden her sones; and her douytris to feendis.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
And thei schedden out innocent blood, the blood of her sones and of her douytris; whiche thei sacrificiden to the grauun ymagis of Chanaan.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
And the erthe was slayn in bloodis, and was defoulid in the werkis of hem; and thei diden fornicacioun in her fyndyngis.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
And the Lord was wrooth bi strong veniaunce ayens his puple; and hadde abhominacioun of his eritage.
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
And he bitook hem in to the hondis of hethene men; and thei that hatiden hem, weren lordis of hem.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
And her enemyes diden tribulacioun to hem, and thei weren mekid vndir the hondis of enemyes;
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
ofte he delyuerede hem. But thei wraththiden hym in her counsel; and thei weren maad low in her wickidnessis.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
And he siye, whanne thei weren set in tribulacioun; and he herde the preyer of hem.
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
And he was myndeful of his testament; and it repentide hym bi the multitude of his merci.
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
And he yaf hem in to mercies; in the siyt of alle men, that hadden take hem.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Oure Lord God, make thou vs saaf; and gadere togidere vs fro naciouns. That we knouleche to thin hooli name; and haue glorie in thi preisyng.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Blessid be the Lord God of Israel fro the world and til in to the world; and al the puple schal seye, Be it don, be it don.

< Zaburi 106 >