< Zaburi 106 >
1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Hallelujah. Oh give thanks unto the Lord; for he is good: for to eternity endureth his kindness.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Who can utter the mighty acts of the Lord? who can publish all his praise?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Happy are those that observe justice, that execute righteousness at all times.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Remember me, O Lord, when thou favorest thy people: oh visit me with thy salvation;
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
That I may look on the happiness of thy elect, that I may rejoice in the joy of thy nation, that I may glorify myself with thy inheritance.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
We have sinned together with our fathers, we have committed iniquity, we have done wickedly.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Our fathers did not reflect on thy wonders in Egypt: they remembered not the multitude of thy kindnesses; but rebelled at the sea, even at the Red Sea.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Nevertheless he saved them for the sake of his name, to make known his might.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
He rebuked the Red Sea also, and it was dried up; and he led them through the depths, as through the wilderness.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
And he saved them from the hand of him that hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
And the waters covered their adversaries: not one of them was left.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Then believed they in his words, they sang his praise.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
Speedily they forgot his works, they waited not for his counsel;
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
And they felt a lustful longing in the wilderness, and tempted God in the desert.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
And he gave them what they had asked; but sent dryness into their soul.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
Moreover they envied Moses in the camp, and Aaron the holy one of the Lord.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
The earth opened and swallowed up Dathan, and covered over the company of Abiram.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
And a fire was kindled in their company: the flame burnt up the wicked.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
They made a calf in Horeb, and bowed themselves down to a molten image.
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
And they exchanged their glory for the similitude of an ox that eateth herbs.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
They forgot God their saviour, who had done great things in Egypt,
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
Wonders in the land of Ham, terrible things by the Red Sea.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
He therefore spoke of destroying them: had not Moses his elect stood in the breach before him, to turn away his fury, that he might not destroy.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
And they despised the pleasant land, they believed not in his word;
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
But they murmured in their tents, they hearkened not unto the voice of the Lord.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
He therefore lifted up his hand against them, to cause them to fall in the wilderness;
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
And to let their seed fall among the nations, and to scatter them in the lands.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
And they joined themselves unto Ba'al-pe'or, and ate the sacrifices of the dead.
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
And they provoked him to anger with their deeds: and there broke in among them the plague.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Then stood up Phinehas, and executed judgment: and the plague was stayed.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
And it was accounted unto him for righteousness, unto all generations for evermore.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
They angered him also at the waters of Meribah, and evil happened to Moses for their sake;
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
Because they had embittered his spirit, and so he spoke thoughtlessly with his lips.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
They did not exterminate the nations, that the Lord had indicated to them;
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
But they mingled themselves among the nations, and learned their doings.
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
And they served their idols, and these became unto them a snare.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
Yea, they sacrificed their sons and their daughters unto the evil spirits;
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
And they shed innocent blood, the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed unto the idols of Canaan: and the land was polluted with blood-guiltiness.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
Thus were they made unclean through their own doings, and went astray with their own deeds.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
therefore was the wrath of the Lord kindled against his people, and be felt disgust for his own inheritance.
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
And he gave them up into the hand of the nations: and there ruled over them those that hated them.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
And their enemies also oppressed them: and they were subdued under their hand.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Many times did he deliver them; but they rebelled with their counsel, and they were brought low through their iniquity.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
Nevertheless he looked on when they were in distress, when he heard their entreaty.
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
And he remembered unto them his covenant, and he bethought himself according to the abundance of his kindnesses;
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
And be caused them to find mercy before all those that had carried them away captive.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Save us, O Lord our God, and gather us from among the nations, to give thanks unto thy holy name, to triumph in thy praise.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Blessed be the Lord the God of Israel from everlasting even to everlasting: and let all the people say, Amen, Hallelujah.