< Zaburi 105 >

1 Mshukuruni Yahwe, liitieni jina lake; myafanye matendo yake yajulikane kati ya mataifa.
ALABAD á Jehová, invocad su nombre: haced notorias sus obras en los pueblos.
2 Mwimbieni yeye, mwimbieni sifa yeye; semeni matendo yake yote ya ajau.
Cantadle, cantadle salmos: hablad de todas sus maravillas.
3 Mjivune katika utakatifu wa jina lake; moyo wao wamtafutao Yahwe ufurahi.
Gloriaos en su santo nombre: alégrese el corazón de los que buscan á Jehová.
4 Mtafuteni Yahwe na nguvu zake; utafuteni uwepo wake siku zote.
Buscad á Jehová, y su fortaleza: buscad siempre su rostro.
5 Kumbukeni mambo ya ajabu aliyoyatenda,
Acordaos de sus maravillas que hizo, de sus prodigios y de los juicios de su boca,
6 miujiza yake na amri zitokazo kinywani mwake, enyi kizazi cha Ibrahimu mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wachaguliwa wake.
Oh vosotros, simiente de Abraham su siervo, hijos de Jacob, sus escogidos.
7 Yeye ni Yahwe, Mungu wetu. Amri zake ziko juu ya nchi yote.
El es Jehová nuestro Dios; en toda la tierra son sus juicios.
8 Naye hulikumbuka agano lake milele, neno alilo amuru kwa ajili ya vizazi elfu.
Acordóse para siempre de su alianza; de la palabra que mandó para mil generaciones,
9 Hulikumbuka agano alilolifanya na Ibrahimu na kiapo alicho mwapia Isaka.
La cual concertó con Abraham; y de su juramento á Isaac.
10 Hiki ndicho alicho mthibitishia Yakobo kama agano na kama agano la milele kwa Israeli.
Y establecióla á Jacob por decreto, á Israel por pacto sempiterno,
11 Alisema, “Nitakupa wewe ardhi ya Kanaani kama sehemu yako ya urithi.”
Diciendo: A ti daré la tierra de Canaán [por] cordel de vuestra heredad.
12 Alisema hili wakati tu walipokuwa wachache katika hesabu, yaani wachahe sana, nao walikuwa wageni katika nchi.
[Esto] siendo ellos pocos hombres en número, y extranjeros en ella.
13 Walienda taifa hadi taifa na kutoka ufalme moja kwenda mwingine.
Y anduvieron de gente en gente, de un reino á otro pueblo.
14 Hakuruhusu yeyote kuwaonea; aliwakemea wafalme kwa ajili yao.
No consintió que hombre los agraviase; y por causa de ellos castigó los reyes.
15 Alisema, “Msiwaguze wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
No toquéis, [dijo], á mis ungidos, ni hagáis mal á mis profetas.
16 Aliita njaa katika nchi; akaondoa upatikanaji wa mkate wote.
Y llamó al hambre sobre la tierra, y quebrantó todo mantenimiento de pan.
17 Akatuma mtu mbele yao; Yusufu aliuzwa kama mtumishi.
Envió un varón delante de ellos, á José, [que] fué vendido por siervo.
18 Miguu yake ilifungwa kwa pingu; alivishwa mnyororo wa chuma shingoni mwake,
Afligieron sus pies con grillos; en hierro fué puesta su persona.
19 mpaka wakati wa maneno yake ulipotimia, nalo neno la Yahwe lilimjaribu.
Hasta la hora que llegó su palabra, el dicho de Jehová le probó.
20 Mfalme alituma watumishi kumfungua; mtawala wa watu alimuweka huru.
Envió el rey, y soltóle; el señor de los pueblos, y desatóle.
21 Alimuweka kuwa msimamizi wa nyumba yake kama mtawala wa mali zake zote
Púsolo por señor de su casa, y por enseñoreador en toda su posesión;
22 kuwaelekeza wakuu kama alivyopenda na kuwafundisha viongozi wake hekima.
Para que reprimiera á sus grandes como él quisiese, y á sus ancianos enseñara sabiduría.
23 Kisha Israeli iliingia Misri, na Yakobo aliishi kwa muda katika nchi ya Hamu.
Después entró Israel en Egipto, y Jacob fué extranjero en la tierra de Châm.
24 Yahwe aliwajalia watu wake wazae sana, na aliwafanya wenye nguvu kuliko adui zao.
Y multiplicó su pueblo en gran manera, é hízolo fuerte más que sus enemigos.
25 Alisababisha adui zao wawachukie watu wake, na kuwatendea visivyo watumishi wake.
Volvió el corazón de ellos para que aborreciesen á su pueblo, para que contra sus siervos pensasen mal.
26 Alimtuma Musa, mtumishi wake, na Haruni, ambaye alikwisha mchagua.
Envió á su siervo Moisés, [y] á Aarón al cual escogió.
27 Walifanya ishara zake kati ya Wamisri na maajabu yake katika ya nchi ya Hamu.
Pusieron en ellos las palabras de sus señales, y sus prodigios en la tierra de Châm.
28 Alituma giza na likaifanya nchi hiyo kuwa giza, lakini watu wake hawakutii amri zake.
Echó tinieblas, é hizo oscuridad; y no fueron rebeldes á su palabra.
29 Aligeuza maji kuwa damu na aliua samaki wao.
Volvió sus aguas en sangre, y mató sus pescados.
30 Nchi yao ilijaa vyura, hata katika vyumba vya watawala wao.
Produjo su tierra ranas, [aun] en las cámaras de sus reyes.
31 Alisema, na makundi ya inzi na chawa wakaja mjini mwote.
Dijo, y vinieron enjambres de moscas, y piojos en todo su término.
32 Aliigeuza mvua yao kuwa mvua ya mawe, pamoja na miali ya moto juu ya ardhi yao.
Volvió en su tierra sus lluvias en granizo, [y] en fuego de llamaradas.
33 Aliiharibu mizabibu yao na mitini yao; akaivunja miti ya mji wao.
E hirió sus viñas y sus higueras, y quebró los árboles de su término.
34 Alisema, na nzige wakaja, nzige wengi sana.
Dijo, y vinieron langostas, y pulgón sin número;
35 Nzige walikula mboga zao zote za majani katika nchi yao. Walikula mazao yote ardhini.
Y comieron toda la hierba de su país, y devoraron el fruto de su tierra.
36 Aliua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao, malimbuko ya nguvu zao.
Hirió además á todos los primogénitos en su tierra, el principio de toda su fuerza.
37 Aliwatoa nje Waisraeli wakiwa na fedha na dhahabu; hakuna mmoja wa kabila lake aliyejikwaa njiani.
Y sacólos con plata y oro; y no hubo en sus tribus enfermo.
38 Misri ilifurahi walipoondoka, maana Wamisri waliwaogopa.
Egipto se alegró de que salieran; porque su terror había caído sobre ellos.
39 Alitandaza wingu liwafunike na alifanya moto uwaangazie wakati wa usiku.
Extendió una nube por cubierta, y fuego para alumbrar la noche.
40 Waisraeli waliomba chakula, naye aliwaletea kware na aliwatosheleza kwa mkate kutoka mbiguni.
Pidieron, é hizo venir codornices; y saciólos de pan del cielo.
41 Aliugawa mwamba, maji yalimwagika kutoka humo; yalitiririka katika jangwa kama mto.
Abrió la peña, y fluyeron aguas; corrieron por los secadales [como] un río.
42 Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu aliyoifanya kwa Ibrahimu mtumishi wake.
Porque se acordó de su santa palabra, [dada] á Abraham su siervo.
43 Aliwaongoza watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za ushindi.
Y sacó á su pueblo con gozo; con júbilo á sus escogidos.
44 Aliwapa nchi za mataifa; walichukua milki ya mali za watu
Y dióles las tierras de las gentes; y las labores de las naciones heredaron:
45 ili waweze kushika amri zake na kutii sheria zake. Msifuni Yahwe.
Para que guardasen sus estatutos, y observasen sus leyes. Aleluya.

< Zaburi 105 >