< Zaburi 103 >
1 Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote, na vyote vilivyomo ndani yangu, nitalisifu jina lake takatifu.
達味作。我的靈魂,請向上主讚頌,我的五內,請向主名讚頌。
2 Maishani mwangu mwote nitamsifu Yahwe, na kukumbuka matendo yake yote mazuri.
我的靈魂,請向上主讚頌,請你不要忘記他的恩寵。
3 Yeye husamehe dhambi zako zote; huponya magonjwa yako yote.
是他赦免了你的各種愆尤,是他治愈了你的一切病苦,
4 Huukomboa uhai wako dhidi ya uharubifu; hukuvika taji kwa uaminifu wa agano lake na hutenda kwa rehema.
是他叫你的性命在死亡中得到保全,是他用仁慈以及愛情給你作了冠冕,
5 Huyatosheleza maisha yako kwa mambo mema ili kwamba ujana wako ufanywe upya kama tai.
是他賞賜你一生幸福滿盈,是他使你的青春更新如鷹。
6 Yahwe hutenda yaliyo haki naye hutenda hukumu ya haki kwa ajili ya wote walio onewa.
上主常行正義的工作,為受壓迫者主持公道。
7 Alimjulisha Musa njia zake, matendo yake kwa uzao wa Israeli.
上主曾將自己的道路告知梅瑟,給以色列子民彰顯自己的功績。
8 Yahwe ni wa huruma na neema; ni mvumilivu; ana agano kuu la uaminifu.
上主富於仁慈寬恕,極其慈悲,遲於發怒。
9 Hataadhibu siku zote; hakasiriki siku zote.
他決不會常常責問,也決不會世世憤恨。
10 Hatushughulikii sisi kama dhambi zetu zinavyostahili au kutulipa kulingana na uhitaji wa dhambi zetu.
他沒有按我們的罪惡對待我們,也沒有照我們的過犯報復我們。
11 Kama mbingu zilivyo juu zaidi ya nchi, ndivyo ulivyo ukuu wa uaminifu wa agano lake kwao wale wanaomcha yeye.
就如上天距離下地有多麼高,他待敬畏他者的慈愛也多高;
12 Kama vile mashariki ilivyo mbali na magharibi, hivi ndivyo ameondoa hatia zetu za dhambi zetu mbali nasi.
就如東方距離西方有多麼遠,他使我們的罪離我們也多遠;
13 Kama vile baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Yahwe alivyo na huruma kwao wamchao.
就如父親怎樣憐愛自己兒女們,上主也怎樣憐愛敬畏自己的人們。
14 Maana anajua tulivyo umbwa; anajua kuwa tu mavumbi.
他原知道我們怎樣形成,也記得我們不過是灰塵。
15 Kama ilivyo kwa mwanadamu, siku zake ni kama majani; hustawi kama ua katika shamba.
世人的歲月與青草無異,又像田野的花,茂盛一時,
16 Upepo hulipiga, nalo hutoweka, na hakuna hata mmoja awezaye kuelezea mahali lilipokua.
只要輕風吹過,他就不復存在,沒有人認得出他原有的所在。
17 Lakini agano la uaminifu wa Yahwe uko kwa wale wamchao yeye milele hata milele. Haki yake ni endelevu kwa uzao wao.
但上主的慈愛永遠臨於敬畏他的人,他的正義永遠臨於他們的子子孫孫:
18 Wanashika agano lake na kukumbuka kutii maagizo yake.
就是臨於那些遵守他盟約的人,和那些懷念並履行他誡命的人。
19 Yahwe ameweka kiti chake cha enzi mbinguni, na ufalme wake watawala juu ya kila mtu.
上主在天上立定了自己的寶位,天下的萬物都屬他的王權統治。
20 Msifuni Yahwe, enyi malaika zake, ninyi hodari wenye nguvu na mtendao neno lake, na kutii sauti ya neno lake.
上主的眾天使,請你們讚美上主,你們是執行他命令的大能臣僕,又是服從上主聖言的聽命公侯;
21 Msifuni Yahwe, enyi jeshi la malaika wote, ninyi ni watumishi mfanyao mapenzi yake.
上主的眾天使,請讚美上主,您們是奉行祂旨意的忠僕,
22 Msifuni Yahwe, viumbe wake wote, mahali popote atawalapo. Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote.
上主所有的一切受造物,在祂權限所達的各處,請您們大家都讚美上主。我的靈魂請您讚美上主!