< Zaburi 102 >
1 Sikia maombi yangu, Ee Yahwe; sikia kulia kwangu kwako.
ヱホバよわが祈をききたまへ 願くはわが號呼のこゑの御前にいたらんことを
2 Usiufiche uso wako mbali nami wakati wa shida. Unisikilize. Nikuitapo, unijibu upesi.
わが窮苦の日みかほを蔽ひたまふなかれ なんぢの耳をわれにかたぶけ 我がよぶ日にすみやかに我にこたへたまへ
3 Kwa maana siku zangu zinapita kama moshi, na mifupa yangu kama moto.
わがもろもろの日は煙のごとくきえ わが骨はたきぎのごとく焚るるなり
4 Moyo wangu umeumizwa na niko kama majani yaliyo kauka. Ninasahau kula chakula chochote.
わがこころは草のごとく撃れてしほれたり われ糧をくらふを忘れしによる
5 Kwa muendelezo wa kuugua kwangu, nimekonda sana.
わが歎息のこゑによりてわが骨はわが肉につく
6 Niko kama mwali wa jangwani; nimekuwa kama bundi magofuni.
われは野の鸅鸕のごとく荒たる跡のふくろふのごとくになりぬ
7 Ninalala macho kama shomoro faraghani, pekeyake juu ya paa.
われ醒てねぶらず ただ友なくして屋蓋にをる雀のごとくなれり
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; wale wanao nidhihaki hutumia jina langu katika laana.
わが仇はひねもす我をそしる 猖狂ひて我をせむるもの我をさして誓ふ
9 Ninakula majivu kama mkate na kuchanganya kinywaji changu kwa machozi.
われは糧をくらふごとくに灰をくらひ わが飮ものには涙をまじへたり
10 Kwa sababu ya hasira yako kali, umeniinua juu kunitupa chini.
こは皆なんぢの怒と忿恚とによりてなり なんぢ我をもたげてなげすて給へり
11 Siku zangu ni kama kivuli kanachofifia, na ninanyauka kama majani.
わが齡はかたぶける日影のごとし またわれは草のごとく萎れたり
12 Lakini wewe, Yahwe, unaishi milele, na kumbukumbu lako ni kwa vizazi vyote.
されどヱホバよなんぢは永遠にながらへ その名はよろづ世にながらへん
13 Wewe utasimama na kuirehemu Sayuni. Sasa ni wakati wa mkurehemu yeye. Wakati ulio teuliwa umefika.
なんぢ起てシオンをあはれみたまはん そはシオンに恩惠をほどこしたまふときなり そのさだまれる期すでに來れり
14 Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake pendwa na kuyaonea huruma mavumbi ya magofu yake.
なんぢの僕はシオンの石をもよろこび その塵をさへ愛しむ
15 Mataifa wataliheshimu jina lako, Yahwe, na wafalme wote wa nchi watauheshimu utukufu wako.
もろもろの國はヱホバの名をおそれ 地のもろもろの王はその榮光をおそれん
16 Yahwe ataijenga tena Sayuni na ataonekana katika utukufu wake.
ヱホバはシオンをきづき榮光をもてあらはれたまへり
17 Wakati huo, atajibu maombi ya fukara; hatayakataa maombi yao.
ヱホバは乏しきものの祈をかへりみ彼等のいのりを藐しめたまはざりき
18 Hii itaandikwa kwa ajili ya vizazi vijavyo, na watu ambao bado hawajazaliwa watamsifu Yahwe.
來らんとするのちの世のためにこの事をしるさん 新しくつくられたる民はヤハをほめたたふべし
19 Maana ametazama chini toka mahali pa juu patakatifu;
ヱホバその聖所のたかき所よりみおろし天より地をみたまへり
20 Toka mbinguni Yahwe ameiangalia nchi, ili kusikia kuugua kwa wafungwa, kuwafungua waliohukumiwa kufa.
こは俘囚のなげきをきき死にさだまれる者をときはなち
21 Kisha watu watalitangaza jina la Yahwe katika Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu
人々のシオンにてヱホバの名をあらはしヱルサレムにてその頌美をあらはさんが爲なり
22 pindi mataifa na falme watakapokusanyika pamoja kumtumikia Yahwe.
かかる時にもろもろの民もろもろの國つどひあつまりてヱホバに事へまつらん
23 Amechukua nguvu zangu katikati ya siku zangu za kuishi, amezifupisha siku zangu.
ヱホバはわがちからを途にておとろへしめ わが齢をみじかからしめ給へり
24 Nilisema, “Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; wewe uko hapa hata kizazi chote.
我いへりねがはくはわが神よわがすべての日のなかばにて我をとりさりたまふなかれ 汝のよはひは世々かぎりなし
25 Tangu zama za kale wewe uliiweka nchi mahali pake; mbingu ni kazi ya mikono yako.
汝いにしへ地の基をすゑたまへり 天もまたなんぢの手の工なり
26 Mbingu na nchi zitaangamia lakini wewe utabaki; zitachakaa kama mavazi; utaziondoa kama watu waondoavyo mavazi yaliyo chakaa, nazo hazitaonekana tena.
これらは亡びん されど汝はつねに存らへたまはん これらはみな衣のごとくふるびん 汝これらを袍のごとく更たまはん されば彼等はかはらん
27 Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitakuwa na mwisho.
然れども汝はかはることなし なんぢの齢はをはらざるなり
28 Watoto wa watumishi wako wataendelea kuishi, na uzao wao utaishi katika uwepo wako.
汝のしもべの子輩はながらへん その裔はかたく前にたてらるべし