< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
Psaume de David. Je veux chanter la bonté et la justice; C'est toi, ô Éternel, que je célébrerai.
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
Je m'appliquerai à suivre la voie de l'intégrité. Quand viendras-tu à moi? Je donnerai l'exemple d'une conduite intègre. Au sein de ma famille.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
Je chasserai de mon esprit toute pensée coupable. J'ai en horreur les actes d'iniquité: Ils n'ont aucun attrait pour moi.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
Le coeur pervers s'éloignera de moi; Je ne connaîtrai point le mal.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
J'anéantirai celui qui parle en secret contre son prochain. Je ne supporterai pas le regard hautain. Ni le coeur enflé d'orgueil.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
J'aurai les yeux sur les fidèles du pays, Pour les faire demeurer avec moi. Celui qui marche dans l'intégrité, celui-là me servira.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
Celui qui use de tromperie n'habitera pas dans ma maison; Celui qui profère le mensonge Ne subsistera pas devant mes yeux.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
Chaque matin, je détruirai tous les méchants du pays, Afin que tous les ouvriers d'iniquité Disparaissent de la cité de l'Éternel.

< Zaburi 101 >