< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
A Psalm by David. I will sing of loving kindness and justice. To you, LORD, I will sing praises.
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
I will be careful to live a blameless life. When will you come to me? I will walk within my house with a blameless heart.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I will set no vile thing before my eyes. I hate the deeds of faithless men. They will not cling to me.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
A perverse heart will be far from me. I will have nothing to do with evil.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
I will silence whoever secretly slanders his neighbour. I won’t tolerate one who is arrogant and conceited.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
My eyes will be on the faithful of the land, that they may dwell with me. He who walks in a perfect way, he will serve me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
He who practices deceit won’t dwell within my house. He who speaks falsehood won’t be established before my eyes.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
Morning by morning, I will destroy all the wicked of the land, to cut off all the workers of iniquity from the LORD’s city.

< Zaburi 101 >