< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
“A psalm of David.” I will sing of mercy and justice; To thee, O LORD! will I sing!
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
I will have regard to the way of uprightness: When thou shalt come to me, I will walk within my house with an upright heart.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I will set no wicked thing before mine eyes; I hate the work of evil-doers; It shall not cleave to me.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
The perverse in heart shall be far from me; I will not know a wicked person.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
Whoso slandereth his neighbor in secret, him will I cut off; Him that hath a haughty look and a proud heart I will not endure.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
Mine eyes shall be upon the faithful of the land, that they may dwell with me; He that walketh in the way of uprightness shall serve me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
He who practiseth deceit shall not dwell in my house; He who telleth lies shall not remain in my sight.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
Every morning will I destroy the wicked of the land, That I may cut off all evil-doers from the city of the LORD.

< Zaburi 101 >