< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
A psalm for David himself. Mercy and judgment I will sing to thee, O Lord: I will sing,
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
And I will understand in the unspotted way, when thou shalt come to me. I walked in the innocence of my heart, in the midst of my house.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I did not set before my eyes any unjust thing: I hated the workers of iniquities.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
The perverse heart did not cleave to me: and the malignant, that turned aside from me, I would not know.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
The man that in private detracted his neighbour, him did I persecute. With him that had a proud eye, and an unsatiable heart, I would not eat.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
My eyes were upon the faithful of the earth, to sit with me: the man that walked in the perfect way, he served me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
He that worketh pride shall not dwell in the midst of my house: he that speaketh unjust things did not prosper before my eyes.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
In the morning I put to death all the wicked of the land: that I might cut off all the workers of iniquity from the city of the Lord.

< Zaburi 101 >