< Zaburi 100 >
1 Mpigieni Yahwe kelele za furaha, enyi nchi yote.
稱謝詩。 普天下當向耶和華歡呼!
2 Mtumikieni Yahwe kwa furaha; njoni mbele zake mkiimba kwa furaha.
你們當樂意事奉耶和華, 當來向他歌唱!
3 Mjue kuwa Yahwe ni Mungu; alituumba, na sisi tu wake. Tu watu wake na kondoo wa malisho yake.
你們當曉得耶和華是上帝! 我們是他造的,也是屬他的; 我們是他的民,也是他草場的羊。
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na nyuani mwake kwa kusifu. Mshukuruni yeye na litukuzeni jina lake.
當稱謝進入他的門; 當讚美進入他的院。 當感謝他,稱頌他的名!
5 Maana Yahwe ni mwema; uaminifu wa agano lake wadumu milele na uaminifu wake vizazi na vizazi vyote.
因為耶和華本為善。 他的慈愛存到永遠; 他的信實直到萬代。