< Zaburi 100 >
1 Mpigieni Yahwe kelele za furaha, enyi nchi yote.
普世大地請向上主歡呼,
2 Mtumikieni Yahwe kwa furaha; njoni mbele zake mkiimba kwa furaha.
要興高彩烈地事奉上主;走到上主面前,應該歡呼!
3 Mjue kuwa Yahwe ni Mungu; alituumba, na sisi tu wake. Tu watu wake na kondoo wa malisho yake.
您們應該明認雅威就是天主,祂造成了我們,我們非祂莫屬;我們是祂的人民,是祂牧場的羊隊。
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na nyuani mwake kwa kusifu. Mshukuruni yeye na litukuzeni jina lake.
高唱感恩歌,邁向祂的大門,吟詠讚美詩,進入祂的庭院,向祂致謝,讚美祂的聖名。
5 Maana Yahwe ni mwema; uaminifu wa agano lake wadumu milele na uaminifu wake vizazi na vizazi vyote.
因為上主良善寬仁,祂的慈愛直到永恒,祂的忠信世世常存。