< Zaburi 10 >
1 Kwa nini, Yahweh, unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati wa shida?
Pourquoi te tiens-tu à l'écart, Yahvé? Pourquoi vous cachez-vous dans les moments difficiles?
2 Kwa sababu ya majivuno yao, watu waovu waawakimbiza wanyonge; Basi tafadhari uwafanye waovu kunaswa kwa mipango yao wenyewe walioipanga.
Dans leur arrogance, les méchants traquent les faibles. Ils sont pris dans les combines qu'ils conçoivent.
3 Kwa kuwa mtu mwovu hujivuna kwa tamaa yake ya ndani; yeye hufurahisha tamaa na kumtusi Yahweh.
Car le méchant se vante des désirs de son cœur. Il bénit les cupides et condamne Yahvé.
4 Mtu mwovu ameinua uso wake; naye hamtafuti Mungu. Yeye hamfikilii Mungu kamwe kwa kuwa hamjali kabisa Mungu.
Le méchant, dans l'orgueil de son visage, n'a pas de place dans ses pensées pour Dieu.
5 Yeye yuko salama wakati wote, amri zako za haki ziko juu sana kwake; naye huwadharau adui zake wote.
Ses voies sont prospères en tout temps. Il est arrogant, et vos lois sont loin de sa vue. Quant à tous ses adversaires, il se moque d'eux.
6 Yeye husema moyoni mwake, “Siwezi kamwe kushindwa; katika kizazi chote sitakutana na shida.”
Il dit en son cœur: « Je ne serai pas ébranlé. Pour les générations à venir, je n'aurai aucun problème. »
7 Mdomoni mwake kumejaa kulaani na udanganyifu, maneno yenye sumu; ulimi wake unajeruhi na kuharibu.
Sa bouche est pleine de malédiction, de tromperie et d'oppression. Sous sa langue se cachent la malice et l'iniquité.
8 Yeye husubilia kwenye shambulio karibu na kijiji; mahali pa siri huwauwa watu wasio na hatia; macho yake huwatazama wasionahatia.
Il se tient à l'affût près des villages. Depuis des embuscades, il assassine les innocents. Ses yeux sont secrètement tournés vers les personnes sans défense.
9 Hujibanza mahari pa siri kama simba katika kichaka; yeye hulala akisubiri kumkamata mnyonge. Humkamata pale anapokwisha mweka mtegoni mwake.
Il se tapit en secret comme un lion dans son embuscade. Il est à l'affût pour attraper les impuissants. Il attrape les impuissants quand il les prend dans son filet.
10 Wanyonge wake hugandamizwa chini na kupigwa; wao huangukia katika mtego imara.
Les impuissants sont écrasés. Ils s'effondrent. Ils tombent sous sa coupe.
11 Yeye husema katika moyo wake, “Mungu amesahau; huficha uso wake; hawezi kujishughulisha kutazama.”
Il dit dans son cœur: « Dieu a oublié. Il cache son visage. Il ne le verra jamais. »
12 Inuka, Yahweh! Inua mkono wako, Mungu! Usiwasahau wanyonge.
Lève-toi, Yahvé! Dieu, lève ta main! N'oubliez pas les impuissants.
13 Kwa nini mtu mwovu anamkataa Mungu na kusema moyoni mwake, “Hautanipata katika hatia?”
Pourquoi le méchant condamne-t-il Dieu, et dire dans son cœur, « Dieu ne me demandera pas de comptes »?
14 Umeona, maana mara zote unaangalia mtu aletaye madhara na jeuri. Mtu asiye na msaada hukuachia nafsi yake; maana wewe huwaokoa yatima.
Mais vous voyez la détresse et le chagrin. Vous le considérez pour le prendre en main. Vous aidez la victime et l'orphelin.
15 vunja mkono wa mwovu lo na mtu mwovu. Umuajibishe kwa matendo yake maovu, ambayo kwayo alifikiri hautayagundua.
Brisez le bras des méchants. Quant à l'homme mauvais, cherche sa méchanceté jusqu'à ce que tu n'en trouves aucune.
16 Yahweh ni mfalme milele daima; mataifa yanaondolewa katika aridhi yake.
Yahvé est roi pour les siècles des siècles! Les nations périront hors de son pays.
17 Yahweh, umesikia uhitaji wa wanyonge; nawe umeitia nguvu mioyo yao, wewe unasikia maombi;
Yahvé, tu as entendu le désir des humbles. Vous allez préparer leur cœur. Tu feras en sorte que ton oreille entende,
18 Unawatetea yatima na wanyonge ili kusudi pasiwepo na mtu katika dunia hii atakaye leta hofu tena.
pour juger l'orphelin et l'opprimé, pour que l'homme qui est de la terre ne soit plus terrifié.