< Zaburi 10 >
1 Kwa nini, Yahweh, unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati wa shida?
Why, O LORD, do You stand far off? Why do You hide in times of trouble?
2 Kwa sababu ya majivuno yao, watu waovu waawakimbiza wanyonge; Basi tafadhari uwafanye waovu kunaswa kwa mipango yao wenyewe walioipanga.
In pride the wicked pursue the needy; let them be caught in the schemes they devise.
3 Kwa kuwa mtu mwovu hujivuna kwa tamaa yake ya ndani; yeye hufurahisha tamaa na kumtusi Yahweh.
For the wicked man boasts in the cravings of his heart; he blesses the greedy and reviles the LORD.
4 Mtu mwovu ameinua uso wake; naye hamtafuti Mungu. Yeye hamfikilii Mungu kamwe kwa kuwa hamjali kabisa Mungu.
In his pride the wicked man does not seek Him; in all his schemes there is no God.
5 Yeye yuko salama wakati wote, amri zako za haki ziko juu sana kwake; naye huwadharau adui zake wote.
He is secure in his ways at all times; Your lofty judgments are far from him; he sneers at all his foes.
6 Yeye husema moyoni mwake, “Siwezi kamwe kushindwa; katika kizazi chote sitakutana na shida.”
He says to himself, “I will not be moved; from age to age I am free of distress.”
7 Mdomoni mwake kumejaa kulaani na udanganyifu, maneno yenye sumu; ulimi wake unajeruhi na kuharibu.
His mouth is full of cursing, deceit, and violence; trouble and malice are under his tongue.
8 Yeye husubilia kwenye shambulio karibu na kijiji; mahali pa siri huwauwa watu wasio na hatia; macho yake huwatazama wasionahatia.
He lies in wait near the villages; in ambush he slays the innocent; his eyes watch in stealth for the helpless.
9 Hujibanza mahari pa siri kama simba katika kichaka; yeye hulala akisubiri kumkamata mnyonge. Humkamata pale anapokwisha mweka mtegoni mwake.
He lies in wait like a lion in a thicket; he lurks to seize the oppressed; he catches the lowly in his net.
10 Wanyonge wake hugandamizwa chini na kupigwa; wao huangukia katika mtego imara.
They are crushed and beaten down; the hapless fall prey to his strength.
11 Yeye husema katika moyo wake, “Mungu amesahau; huficha uso wake; hawezi kujishughulisha kutazama.”
He says to himself, “God has forgotten; He hides His face and never sees.”
12 Inuka, Yahweh! Inua mkono wako, Mungu! Usiwasahau wanyonge.
Arise, O LORD! Lift up Your hand, O God! Do not forget the helpless.
13 Kwa nini mtu mwovu anamkataa Mungu na kusema moyoni mwake, “Hautanipata katika hatia?”
Why has the wicked man renounced God? He says to himself, “You will never call me to account.”
14 Umeona, maana mara zote unaangalia mtu aletaye madhara na jeuri. Mtu asiye na msaada hukuachia nafsi yake; maana wewe huwaokoa yatima.
But You have regarded trouble and grief; You see to repay it by Your hand. The victim entrusts himself to You; You are the helper of the fatherless.
15 vunja mkono wa mwovu lo na mtu mwovu. Umuajibishe kwa matendo yake maovu, ambayo kwayo alifikiri hautayagundua.
Break the arm of the wicked and evildoer; call him to account for his wickedness until none is left to be found.
16 Yahweh ni mfalme milele daima; mataifa yanaondolewa katika aridhi yake.
The LORD is King forever and ever; the nations perish from His land.
17 Yahweh, umesikia uhitaji wa wanyonge; nawe umeitia nguvu mioyo yao, wewe unasikia maombi;
You have heard, O LORD, the desire of the humble; You will strengthen their hearts. You will incline Your ear,
18 Unawatetea yatima na wanyonge ili kusudi pasiwepo na mtu katika dunia hii atakaye leta hofu tena.
to vindicate the fatherless and oppressed, that the men of the earth may strike terror no more.