< Mithali 1 >
1 Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
Los proverbios de Salomón, hijo de David, rey de Israel:
2 Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
Para conocer sabiduría y castigo; para entender las razones prudentes;
3 ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
para recibir el castigo de prudencia, justicia, juicio y equidad;
4 Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
para dar prudencia a los simples, y a los jóvenes inteligencia y consejo.
5 Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
Si el sabio los oyere, aumentará la doctrina; y el entendido adquirirá consejo;
6 kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
para entender parábola y declaración; palabras de sabios, y sus enigmas.
7 Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
El principio del conocimiento es el temor del SEÑOR; los locos despreciaron la sabiduría y el castigo.
8 Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
Oye, hijo mío, el castigo de tu padre, y no deseches la ley de tu madre;
9 zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
porque aumento de gracia serán a tu cabeza, y protección a tu cuello.
10 Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
Hijo mío, si los pecadores te quisieren engañar, no consientas.
11 Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
Si dijeren: Ven con nosotros, espiemos a alguno para matarle, acechemos al inocente sin razón;
12 Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni. (Sheol )
los tragaremos vivos como el sepulcro, y enteros, como los que caen en un abismo; (Sheol )
13 Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
hallaremos riquezas de toda clase, llenaremos nuestras casas de despojos;
14 Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
echa tu suerte entre nosotros; tengamos todos una bolsa,
15 Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;
hijo mío, no andes en camino con ellos; aparta tu pie de sus veredas;
16 miguu ya hukimbilia mabaya na huharakisha kumwaga damu.
porque sus pies correrán al mal, e irán presurosos a derramar sangre.
17 Kwa kuwa haina maana kumtegea ndege mtego wakati ndege anaona.
Porque en vano se tenderá la red ante los ojos de toda ave;
18 Watu hawa huvizia kujiua wenyewe—wanatega mtego kwa ajili yao wenyewe.
mas ellos a su propia sangre espían, y a sus propias almas ponen asechanza.
19 Ndivyo zilivyo njia za kila ambaye hupata utajiri kwa udhalimu; mapato ya udhalimu huondoa uhai wa wenye utajiri.
Tales son las sendas de todo el que codicia la ganancia, la cual prenderá la vida de sus poseedores.
20 Hekima inalia kwa sauti mtaani, inapaza sauti katika viwanja;
La sabiduría clama de fuera; en las plazas da su voz;
21 katika mitaa inalia kwa sauti kuu, kwenye maingilio ya milango ya mji inasema “
clama en los principales lugares de concurso; en las entradas de las puertas de la ciudad dice sus razones:
22 Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
¿Hasta cuándo, oh simples, amaréis la simpleza, y los burladores desearán el burlar, y los locos aborrecerán la ciencia?
23 Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
Volveos a mi reprensión; he aquí yo os derramaré mi espíritu, y os haré saber mis palabras.
24 Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
Por cuanto llamé, y no quisisteis; extendí mi mano, y no hubo quien escuchase;
25 Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
antes desechasteis todo consejo mío, y no quisisteis mi reprensión;
26 Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
también yo me reiré en vuestra calamidad, y me burlaré cuando os viniere lo que teméis;
27 hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
cuando viniere como una destrucción lo que teméis, y vuestra calamidad llegare como un torbellino; cuando sobre vosotros viniere tribulación y angustia.
28 Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
Entonces me llamarán, y no responderé; me buscarán de mañana, y no me hallarán;
29 Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,
por cuanto aborrecieron el conocimiento, y no escogieron el temor del SEÑOR,
30 hawakufuata mafundisho yangu na wakayadharau masahihisho yangu yote.
ni quisieron mi consejo, y menospreciaron toda reprensión mía.
31 Watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa kwa matunda ya hila zao wenyewe.
Comerán, pues, del fruto de su camino, y de sus consejos se hartarán.
32 kwa maana wajinga hufa wanaporudi nyuma, na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.
Porque el reposo de los ignorantes los matará, y la prosperidad de los locos los echará a perder.
33 Bali kila anisikilizaye ataishi kwa usalama na atapumzika salama pasipo hofu ya maafa.
Mas el que me oyere, habitará confiadamente, y vivirá reposado del temor del mal.