< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
Sapientia ædificavit sibi domum: excidit columnas septem.
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
Immolavit victimas suas, miscuit vinum, et proposuit mensam suam.
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
Misit ancillas suas ut vocarent ad arcem et ad mœnia civitatis.
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
Si quis est parvulus, veniat ad me. Et insipientibus locuta est:
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
Venite, comedite panem meum, et bibite vinum quod miscui vobis.
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Relinquite infantiam, et vivite, et ambulate per vias prudentiæ.
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
Qui erudit derisorem, ipse injuriam sibi facit, et qui arguit impium, sibi maculam generat.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
Noli arguere derisorem, ne oderit te: argue sapientem, et diliget te.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Da sapienti occasionem, et addetur ei sapientia; doce justum, et festinabit accipere.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
Principium sapientiæ timor Domini, et scientia sanctorum prudentia.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
Per me enim multiplicabuntur dies tui, et addentur tibi anni vitæ.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
Si sapiens fueris, tibimetipsi eris; si autem illusor, solus portabis malum.
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
Mulier stulta et clamosa, plenaque illecebris, et nihil omnino sciens,
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
sedit in foribus domus suæ, super sellam in excelso urbis loco,
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
ut vocaret transeuntes per viam, et pergentes itinere suo:
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
Qui est parvulus declinet ad me. Et vecordi locuta est:
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
Aquæ furtivæ dulciores sunt, et panis absconditus suavior.
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol )
Et ignoravit quod ibi sint gigantes, et in profundis inferni convivæ ejus. (Sheol )