< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
LA somma Sapienza ha edificata la sua casa, Ella ha tagliate le sue colonne [in numero di] sette;
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
Ella ha ammazzati i suoi animali, ha temperato il suo vino. Ed anche ha apparecchiata la sua mensa.
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
Ella ha mandate le sue serventi a gridare D'in su i poggiuoli degli alti luoghi della città:
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
Chi [è] scempio? riducasi qua. E a dire a quelli che sono scemi di senno:
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
Venite, mangiate del mio pane, E bevete del vino [che] io ho temperato.
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Lasciate le scempietà, e voi viverete; E camminate per la via della prudenza.
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
Chi corregge lo schernitore [ne] riceve vituperio; E chi riprende l'empio [ne riceve] macchia.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
Non riprender lo schernitore, Che talora egli non ti odii; Riprendi il savio, ed egli ti amerà.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Insegna al savio, ed egli diventerà più savio; Ammaestra il giusto, ed egli crescerà in dottrina.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
Il principio della sapienza [è] il timor del Signore; E la scienza de' santi [è] la prudenza.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
Perciocchè per me ti saranno moltiplicati i giorni, E ti saranno aggiunti anni di vita.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
Se sei savio, sarai savio per te; Se [altresì] sei schernitore, tu solo [ne] porterai [la pena].
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
La donna stolta, strepitosa, Scempia, e che non ha alcuno intendimento,
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
Siede anch'essa all'entrata della sua casa, In seggio, ne' luoghi elevati della città.
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
Per gridare a coloro che passano per la via, Che vanno a dirittura a lor cammino:
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
Chi [è] scempio? riducasi qua. E se vi [è] alcuno scemo di senno, gli dice:
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
Le acque rubate son dolci, E il pane [preso] di nascosto è dilettevole.
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)
Ed egli non sa che là [sono] i morti; [E che] quelli ch'ella ha convitati [son] nel fondo dell'inferno. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >