< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
חכמות בנתה ביתה חצבה עמודיה שבעה
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
טבחה טבחה מסכה יינה אף ערכה שלחנה
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
שלחה נערתיה תקרא-- על-גפי מרמי קרת
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
מי-פתי יסר הנה חסר-לב אמרה לו
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
לכו לחמו בלחמי ושתו ביין מסכתי
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
עזבו פתאים וחיו ואשרו בדרך בינה
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
יסר לץ--לקח לו קלון ומוכיח לרשע מומו
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
אל-תוכח לץ פן-ישנאך הוכח לחכם ויאהבך
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
תן לחכם ויחכם-עוד הודע לצדיק ויוסף לקח
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
תחלת חכמה יראת יהוה ודעת קדשים בינה
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
כי-בי ירבו ימיך ויוסיפו לך שנות חיים
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
אם-חכמת חכמת לך ולצת לבדך תשא
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
אשת כסילות המיה פתיות ובל-ידעה מה
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
וישבה לפתח ביתה-- על-כסא מרמי קרת
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
לקרא לעברי-דרך המישרים ארחותם
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
מי-פתי יסר הנה וחסר-לב ואמרה לו
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
מים-גנובים ימתקו ולחם סתרים ינעם
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)
ולא-ידע כי-רפאים שם בעמקי שאול קראיה (Sheol h7585)

< Mithali 9 >