< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
Wisdom has built her house, she has hewn out her seven pillars:
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
She has killed her beasts; she has mingled her wine; she has also furnished her table.
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
She has sent forth her maidens: she cries upon the highest places of the city,
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
Whoso is simple, let him turn in here: as for him that wants understanding, she says to him,
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
Come, eat of my bread, and drink of the wine which I have mingled.
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Forsake the foolish, and live; and go in the way of understanding.
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
He that reproves a scorner gets to himself shame: and he that rebukes a wicked man gets himself a blot.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
Reprove not a scorner, lest he hate you: rebuke a wise man, and he will love you.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Give instruction to a wise man, and he will be yet wiser: teach a just man, and he will increase in learning.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
The fear of the LORD is the beginning of wisdom: and the knowledge of the holy is understanding.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
For by me your days shall be multiplied, and the years of your life shall be increased.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
If you be wise, you shall be wise for yourself: but if you scorn, you alone shall bear it.
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
A foolish woman is clamorous: she is simple, and knows nothing.
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
For she sits at the door of her house, on a seat in the high places of the city,
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
To call passengers who go right on their ways:
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
Whoso is simple, let him turn in here: and as for him that wants understanding, she says to him,
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
Stolen waters are sweet, and bread eaten in secret is pleasant.
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol )
But he knows not that the dead are there; and that her guest are in the depths of hell. (Sheol )