< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
Wisedome hath built her house, and hewen out her seuen pillars.
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
She hath killed her vitailes, drawen her wine, and prepared her table.
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
She hath sent forth her maydens and cryeth vpon the highest places of the citie, saying,
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
Who so is simple, let him come hither, and to him that is destitute of wisedome, she sayth,
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
Come, and eate of my meate, and drinke of the wine that I haue drawen.
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Forsake your way, ye foolish, and ye shall liue: and walke in the way of vnderstanding.
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
He that reproueth a scorner, purchaseth to himselfe shame: and he that rebuketh the wicked, getteth himselfe a blot.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
Rebuke not a scorner, least he hate thee: but rebuke a wise man, and he will loue thee.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Giue admonition to the wise, and he will be the wiser: teache a righteous man, and he will increase in learning.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
The beginning of wisedome is the feare of the Lord, and the knowledge of holy things, is vnderstanding.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
For thy dayes shalbe multiplied by me, and the yeeres of thy life shalbe augmented.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
If thou be wise, thou shalt be wise for thy selfe, and if thou be a scorner, thou alone shalt suffer.
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
A foolish woman is troublesome: she is ignorant, and knoweth nothing.
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
But she sitteth at the doore of her house on a seate in the hie places of the citie,
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
To call them that passe by the way, that go right on their way, saying,
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
Who so is simple, let him come hither, and to him that is destitute of wisedome, shee sayth also,
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
Stollen waters are sweete, and hid bread is pleasant.
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)
But he knoweth not, that ye dead are there, and that her ghestes are in the depth of hell. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >