< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
Moudrost vystavěla dům svůj, vytesavši sloupů svých sedm.
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
Zbila dobytek svůj, smísila víno své, stůl také svůj připravila.
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
A poslavši děvečky své, volá na vrchu nejvyšších míst v městě:
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
Kdožkoli jest hloupý, uchyl se sem. Až i bláznivým říká:
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
Poďte, jezte chléb můj, a píte víno, kteréž jsem smísila.
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Opusťte hloupost a živi buďte, a choďte cestou rozumnosti.
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
Kdo tresce posměvače, dochází hanby, a kdo přimlouvá bezbožnému, pohanění.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
Nedomlouvej posměvači, aby tě nevzal v nenávist; přimlouvej moudrému, a bude tě milovati.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Učiň to moudrému, a bude moudřejší; pouč spravedlivého, a bude umělejší.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
Počátek moudrosti jest bázeň Hospodinova, a umění svatých rozumnost.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
Nebo skrze mne rozmnoží se dnové tvoji, a přidánoť bude let života.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
Budeš-li moudrý, sobě moudrý budeš; pakli posměvač, sám vytrpíš.
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
Žena bláznivá štěbetná, nesmyslná, a nic neumí.
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
A sedí u dveří domu svého na stolici, na místech vysokých v městě,
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
Aby volala jdoucích cestou, kteříž přímo jdou stezkami svými, řkuci:
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
Kdo jest hloupý, uchyl se sem. A bláznivému říká:
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
Voda kradená sladší jest, a chléb pokoutní chutnější.
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol )
Ale neví hlupec, že mrtví jsou tam, a v hlubokém hrobě ti, kterýchž pozvala. (Sheol )