< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
智慧建造房屋, 鑿成七根柱子,
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
宰殺牲畜, 調和旨酒, 設擺筵席;
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
打發使女出去, 自己在城中至高處呼叫,
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
說:誰是愚蒙人,可以轉到這裏來! 又對那無知的人說:
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
你們來,吃我的餅, 喝我調和的酒。
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
你們愚蒙人,要捨棄愚蒙, 就得存活,並要走光明的道。
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
指斥褻慢人的,必受辱罵; 責備惡人的,必被玷污。
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
不要責備褻慢人,恐怕他恨你; 要責備智慧人,他必愛你。
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
教導智慧人,他就越發有智慧; 指示義人,他就增長學問。
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
敬畏耶和華是智慧的開端; 認識至聖者便是聰明。
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
你藉着我,日子必增多, 年歲也必加添。
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
你若有智慧,是與自己有益; 你若褻慢,就必獨自擔當。
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
愚昧的婦人喧嚷; 她是愚蒙,一無所知。
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
她坐在自己的家門口, 坐在城中高處的座位上,
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
呼叫過路的, 就是直行其道的人,
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
說:誰是愚蒙人,可以轉到這裏來! 又對那無知的人說:
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
偷來的水是甜的, 暗吃的餅是好的。
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol )
人卻不知有陰魂在她那裏; 她的客在陰間的深處。 (Sheol )