< Mithali 8 >

1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
numquid non sapientia clamitat et prudentia dat vocem suam
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
in summis excelsisque verticibus super viam in mediis semitis stans
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
iuxta portas civitatis in ipsis foribus loquitur dicens
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
o viri ad vos clamito et vox mea ad filios hominum
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
intellegite parvuli astutiam et insipientes animadvertite
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
audite quoniam de rebus magnis locutura sum et aperientur labia mea ut recta praedicent
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
veritatem meditabitur guttur meum et labia mea detestabuntur impium
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
iusti sunt omnes sermones mei non est in eis pravum quid neque perversum
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
recti sunt intellegentibus et aequi invenientibus scientiam
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
accipite disciplinam meam et non pecuniam doctrinam magis quam aurum eligite
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
melior est enim sapientia cunctis pretiosissimis et omne desiderabile ei non potest conparari
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
ego sapientia habito in consilio et eruditis intersum cogitationibus
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
timor Domini odit malum arrogantiam et superbiam et viam pravam et os bilingue detestor
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
meum est consilium et aequitas mea prudentia mea est fortitudo
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
per me reges regnant et legum conditores iusta decernunt
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
per me principes imperant et potentes decernunt iustitiam
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
ego diligentes me diligo et qui mane vigilant ad me invenient me
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
mecum sunt divitiae et gloria opes superbae et iustitia
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
melior est fructus meus auro et pretioso lapide et genimina mea argento electo
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
in viis iustitiae ambulo in medio semitarum iudicii
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
ut ditem diligentes me et thesauros eorum repleam
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
Dominus possedit me initium viarum suarum antequam quicquam faceret a principio
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
ab aeterno ordita sum et ex antiquis antequam terra fieret
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
necdum erant abyssi et ego iam concepta eram necdum fontes aquarum eruperant
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
necdum montes gravi mole constiterant ante colles ego parturiebar
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
adhuc terram non fecerat et flumina et cardines orbis terrae
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
quando praeparabat caelos aderam quando certa lege et gyro vallabat abyssos
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
quando aethera firmabat sursum et librabat fontes aquarum
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
quando circumdabat mari terminum suum et legem ponebat aquis ne transirent fines suos quando adpendebat fundamenta terrae
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
cum eo eram cuncta conponens et delectabar per singulos dies ludens coram eo omni tempore
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
ludens in orbe terrarum et deliciae meae esse cum filiis hominum
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
nunc ergo filii audite me beati qui custodiunt vias meas
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
audite disciplinam et estote sapientes et nolite abicere eam
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
beatus homo qui audit me qui vigilat ad fores meas cotidie et observat ad postes ostii mei
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
qui me invenerit inveniet vitam et hauriet salutem a Domino
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
qui autem in me peccaverit laedet animam suam omnes qui me oderunt diligunt mortem

< Mithali 8 >