< Mithali 8 >

1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
[Numquid non sapientia clamitat, et prudentia dat vocem suam?
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
In summis excelsisque verticibus supra viam, in mediis semitis stans,
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
juxta portas civitatis, in ipsis foribus loquitur, dicens:
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
O viri, ad vos clamito, et vox mea ad filios hominum.
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
Intelligite, parvuli, astutiam, et insipientes, animadvertite.
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
Audite, quoniam de rebus magnis locutura sum, et aperientur labia mea ut recta prædicent.
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
Veritatem meditabitur guttur meum, et labia mea detestabuntur impium.
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
Justi sunt omnes sermones mei: non est in eis pravum quid, neque perversum;
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
recti sunt intelligentibus, et æqui invenientibus scientiam.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
Accipite disciplinam meam, et non pecuniam; doctrinam magis quam aurum eligite:
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
melior est enim sapientia cunctis pretiosissimis, et omne desiderabile ei non potest comparari.]
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
[Ego sapientia, habito in consilio, et eruditis intersum cogitationibus.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
Timor Domini odit malum: arrogantiam, et superbiam, et viam pravam, et os bilingue, detestor.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
Meum est consilium et æquitas; mea est prudentia, mea est fortitudo.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
Per me reges regnant, et legum conditores justa decernunt;
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
per me principes imperant, et potentes decernunt justitiam.
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
Ego diligentes me diligo, et qui mane vigilant ad me, invenient me.
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
Mecum sunt divitiæ et gloria, opes superbæ et justitia.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
Melior est enim fructus meus auro et lapide pretioso, et genimina me argento electo.
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
In viis justitiæ ambulo, in medio semitarum judicii:
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
ut ditem diligentes me, et thesauros eorum repleam.]
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
[Dominus possedit me in initio viarum suarum antequam quidquam faceret a principio.
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
Ab æterno ordinata sum, et ex antiquis antequam terra fieret.
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
Nondum erant abyssi, et ego jam concepta eram: necdum fontes aquarum eruperant,
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
necdum montes gravi mole constiterant: ante colles ego parturiebar.
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
Adhuc terram non fecerat, et flumina, et cardines orbis terræ.
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
Quando præparabat cælos, aderam; quando certa lege et gyro vallabat abyssos;
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
quando æthera firmabat sursum, et librabat fontes aquarum;
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
quando circumdabat mari terminum suum, et legem ponebat aquis, ne transirent fines suos; quando appendebat fundamenta terræ:
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
cum eo eram, cuncta componens. Et delectabar per singulos dies, ludens coram eo omni tempore,
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
ludens in orbe terrarum; et deliciæ meæ esse cum filiis hominum.
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
Nunc ergo, filii, audite me: beati qui custodiunt vias meas.
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
Audite disciplinam, et estote sapientes, et nolite abjicere eam.
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
Beatus homo qui audit me, et qui vigilat ad fores meas quotidie, et observat ad postes ostii mei.
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
Qui me invenerit, inveniet vitam, et hauriet salutem a Domino.
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
Qui autem in me peccaverit, lædet animam suam; omnes qui me oderunt diligunt mortem.]

< Mithali 8 >