< Mithali 8 >

1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
智慧は呼はらざるか 聰明は聲を出さざるか
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
彼は路のほとりの高處また街衢のなかに立ち
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
邑のもろもろの門 邑の口および門々の入口にて呼はりいふ
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
人々よわれ汝をよび 我が聲をもて人の子等をよぶ
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
拙き者よなんぢら聰明に明かなれ 愚なる者よ汝ら明かなる心を得よ
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
汝きけ われ善事をかたらん わが口唇をひらきて正事をいださん
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
我が口は眞實を述べ わが口唇はあしき事を憎むなり
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
わが口の言はみな義し そのうちに虚偽と奸邪とあることなし
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
是みな智者の明かにするところ 知識をうる者の正とするところなり
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
なんぢら銀をうくるよりは我が敎をうけよ 精金よりもむしろ知識をえよ
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
それ智慧は眞珠に愈れり 凡の寳も之に比ぶるに足らず
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
われ智慧は聰明をすみかとし 知識と謹愼にいたる
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
ヱホバを畏るるとは惡を憎むことなり 我は傲慢と驕奢 惡道と虚偽の口とを憎む
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
謀略と聰明は我にあり 我は了知なり 我は能力あり
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
我に由て王者は政をなし 君たる者は義しき律をたて
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
我によりて主たる者および牧伯たちなど凡て地の審判人は世ををさむ
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
われを愛する者は我これを愛す 我を切に求むるものは我に遇ん
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
富と榮とは我にあり 貴き寳と公義とも亦然り
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
わが果は金よりも精金よりも愈り わが利は精銀よりもよし
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
我は義しき道にあゆみ 公平なる路徑のなかを行む
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
これ我を愛する者に貨財をえさせ 又その庫を充しめん爲なり
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
ヱホバいにしへ其御わざをなしそめたまへる前に その道の始として我をつくりたまひき
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
永遠より元始より地の有ざりし前より我は立られ
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
いまだ海洋あらず いまだ大なるみづの泉あらざりしとき我すでに生れ
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
山いまださだめられず 陵いまだ有ざりし前に我すでに生れたり
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
即ち神いまだ地をも野をも地の塵の根元をも造り給はざりし時なり
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
かれ天をつくり海の面に穹蒼を張たまひしとき我かしこに在りき
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
彼うへに雲氣をかたく定め 淵の泉をつよくならしめ
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
海にその限界をたて 水をしてその岸を踰えざらしめ また地の基を定めたまへるとき
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
我はその傍にありて創造者となり 日々に欣び恒にその前に樂み
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
その地にて樂み又世の人を喜べり
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
されば小子等よ いま我にきけ わが道をまもる者は福ひなり
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
敎をききて智慧をえよ 之を棄ることなかれ
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
凡そ我にきき 日々わが門の傍にまち わが戸口の柱のわきにたつ人は福ひなり
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
そは我を得る者は生命をえ ヱホバより恩寵を獲ればなり
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
我を失ふものは自己の生命を害ふ すべて我を惡むものは死を愛するなり

< Mithali 8 >