< Mithali 8 >
1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
La Sapienza forse non chiama e la prudenza non fa udir la voce?
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
In cima alle alture, lungo la via, nei crocicchi delle strade essa si è posta,
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
presso le porte, all'ingresso della città, sulle soglie degli usci essa esclama:
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
«A voi, uomini, io mi rivolgo, ai figli dell'uomo è diretta la mia voce.
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
Imparate, inesperti, la prudenza e voi, stolti, fatevi assennati.
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
Ascoltate, perché dirò cose elevate, dalle mie labbra usciranno sentenze giuste,
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
perché la mia bocca proclama la verità e abominio per le mie labbra è l'empietà.
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
Tutte le parole della mia bocca sono giuste; niente vi è in esse di fallace o perverso;
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
tutte sono leali per chi le comprende e rette per chi possiede la scienza.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
Accettate la mia istruzione e non l'argento, la scienza anziché l'oro fino,
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
perché la scienza vale più delle perle e nessuna cosa preziosa l'uguaglia».
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
Io, la Sapienza, possiedo la prudenza e ho la scienza e la riflessione.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
Temere il Signore è odiare il male: io detesto la superbia, l'arroganza, la cattiva condotta e la bocca perversa.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
A me appartiene il consiglio e il buon senso, io sono l'intelligenza, a me appartiene la potenza.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
Per mezzo mio regnano i re e i magistrati emettono giusti decreti;
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
per mezzo mio i capi comandano e i grandi governano con giustizia.
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
Io amo coloro che mi amano e quelli che mi cercano mi troveranno.
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
Presso di me c'è ricchezza e onore, sicuro benessere ed equità.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
Il mio frutto val più dell'oro, dell'oro fino, il mio provento più dell'argento scelto.
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
Io cammino sulla via della giustizia e per i sentieri dell'equità,
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
per dotare di beni quanti mi amano e riempire i loro forzieri.
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
Il Signore mi ha creato all'inizio della sua attività, prima di ogni sua opera, fin d'allora.
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
Dall'eternità sono stata costituita, fin dal principio, dagli inizi della terra.
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
Quando non esistevano gli abissi, io fui generata; quando ancora non vi erano le sorgenti cariche d'acqua;
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
prima che fossero fissate le basi dei monti, prima delle colline, io sono stata generata.
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
Quando ancora non aveva fatto la terra e i campi, né le prime zolle del mondo;
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
quando egli fissava i cieli, io ero là; quando tracciava un cerchio sull'abisso;
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
quando condensava le nubi in alto, quando fissava le sorgenti dell'abisso;
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
quando stabiliva al mare i suoi limiti, sicché le acque non ne oltrepassassero la spiaggia; quando disponeva le fondamenta della terra,
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
allora io ero con lui come architetto ed ero la sua delizia ogni giorno, dilettandomi davanti a lui in ogni istante;
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
dilettandomi sul globo terrestre, ponendo le mie delizie tra i figli dell'uomo.
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
Ora, figli, ascoltatemi: beati quelli che seguono le mie vie!
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
Ascoltate l'esortazione e siate saggi, non trascuratela!
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
Beato l'uomo che mi ascolta, vegliando ogni giorno alle mie porte, per custodire attentamente la soglia.
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
Infatti, chi trova me trova la vita, e ottiene favore dal Signore;
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
ma chi pecca contro di me, danneggia se stesso; quanti mi odiano amano la morte».