< Mithali 8 >

1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
智慧豈不呼叫? 聰明豈不發聲?
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
她在道旁高處的頂上, 在十字路口站立,
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
在城門旁,在城門口, 在城門洞,大聲說:
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
眾人哪,我呼叫你們, 我向世人發聲。
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
說:愚蒙人哪,你們要會悟靈明; 愚昧人哪,你們當心裏明白。
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
你們當聽,因我要說極美的話; 我張嘴要論正直的事。
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
我的口要發出真理; 我的嘴憎惡邪惡。
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
我口中的言語都是公義, 並無彎曲乖僻。
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
有聰明的,以為明顯, 得知識的,以為正直。
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
你們當受我的教訓,不受白銀; 寧得知識,勝過黃金。
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
因為智慧比珍珠更美; 一切可喜愛的都不足與比較。
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
我-智慧以靈明為居所, 又尋得知識和謀略。
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
敬畏耶和華在乎恨惡邪惡; 那驕傲、狂妄,並惡道, 以及乖謬的口,都為我所恨惡。
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
我有謀略和真知識; 我乃聰明,我有能力。
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
帝王藉我坐國位; 君王藉我定公平。
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
王子和首領, 世上一切的審判官,都是藉我掌權。
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
愛我的,我也愛他; 懇切尋求我的,必尋得見。
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
豐富尊榮在我; 恆久的財並公義也在我。
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
我的果實勝過黃金,強如精金; 我的出產超乎高銀。
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
我在公義的道上走, 在公平的路中行,
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
使愛我的,承受貨財, 並充滿他們的府庫。
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
在耶和華造化的起頭, 在太初創造萬物之先,就有了我。
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
從亙古,從太初, 未有世界以前,我已被立。
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
沒有深淵, 沒有大水的泉源,我已生出。
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
大山未曾奠定, 小山未有之先,我已生出。
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
耶和華還沒有創造大地和田野, 並世上的土質,我已生出。
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
他立高天,我在那裏; 他在淵面的周圍,劃出圓圈。
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
上使穹蒼堅硬, 下使淵源穩固,
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
為滄海定出界限,使水不越過他的命令, 立定大地的根基。
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
那時,我在他那裏為工師, 日日為他所喜愛, 常常在他面前踴躍,
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
踴躍在他為人預備可住之地, 也喜悅住在世人之間。
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
眾子啊,現在要聽從我, 因為謹守我道的,便為有福。
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
要聽教訓就得智慧, 不可棄絕。
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
聽從我、日日在我門口仰望、 在我門框旁邊等候的,那人便為有福。
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
因為尋得我的,就尋得生命, 也必蒙耶和華的恩惠。
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
得罪我的,卻害了自己的性命; 恨惡我的,都喜愛死亡。

< Mithali 8 >