< Mithali 7 >

1 Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
fili mi custodi sermones meos et praecepta mea reconde tibi
2 Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
serva mandata mea et vives et legem meam quasi pupillam oculi tui
3 Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
liga eam in digitis tuis scribe illam in tabulis cordis tui
4 Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
dic sapientiae soror mea es et prudentiam voca amicam tuam
5 ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
ut custodiat te a muliere extranea et ab aliena quae verba sua dulcia facit
6 Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
de fenestra enim domus meae per cancellos prospexi
7 Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
et video parvulos considero vecordem iuvenem
8 Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
qui transit in platea iuxta angulum et propter viam domus illius graditur
9 Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
in obscuro advesperascente die in noctis tenebris et caligine
10 Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
et ecce mulier occurrit illi ornatu meretricio praeparata ad capiendas animas garrula et vaga
11 Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
quietis inpatiens nec valens in domo consistere pedibus suis
12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
nunc foris nunc in plateis nunc iuxta angulos insidians
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
adprehensumque deosculatur iuvenem et procaci vultu blanditur dicens
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
victimas pro salute debui hodie reddidi vota mea
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
idcirco egressa sum in occursum tuum desiderans te videre et repperi
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
intexui funibus lectum meum stravi tapetibus pictis ex Aegypto
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
aspersi cubile meum murra et aloe et cinnamomo
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
veni inebriemur uberibus donec inlucescat dies et fruamur cupitis amplexibus
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
non est enim vir in domo sua abiit via longissima
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
sacculum pecuniae secum tulit in die plenae lunae reversurus est domum suam
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
inretivit eum multis sermonibus et blanditiis labiorum protraxit illum
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
statim eam sequitur quasi bos ductus ad victimam et quasi agnus lasciviens et ignorans quod ad vincula stultus trahatur
23 mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
donec transfigat sagitta iecur eius velut si avis festinet ad laqueum et nescit quia de periculo animae illius agitur
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
nunc ergo fili audi me et adtende verba oris mei
25 Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
ne abstrahatur in viis illius mens tua neque decipiaris semitis eius
26 Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
multos enim vulneratos deiecit et fortissimi quique interfecti sunt ab ea
27 Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
viae inferi domus eius penetrantes interiora mortis (Sheol h7585)

< Mithali 7 >