< Mithali 7 >
1 Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
Mon fils, honore le Seigneur, et tu seras bon; et n'aie point d'autre crainte.
2 Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
Garde mes préceptes, et tu vivras; et mes paroles, comme la prunelle de tes yeux,
3 Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
attache-les autour de tes doigts; grave-les sur la table de ton cœur.
4 Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
Dis que la sagesse est ta sœur, et fais de la prudence ton amie;
5 ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
afin qu'elle te garde de la femme étrangère et perverse, lorsqu'elle te provoquera avec des paroles flatteuses.
6 Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
Car de sa fenêtre elle se penche sur les places publiques
7 Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
pour voir un fils des insensés, un jeune homme pauvre d'intelligence,
8 Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
passant à l'angle de la rue près de sa maison, et parlant
9 Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
dans l'obscurité du soir, au moment du calme de la nuit et des ténèbres;
10 Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
et la femme descend à sa rencontre; elle a cette beauté de courtisane qui fait tressaillir le cœur des adolescents
11 Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
elle est volage et luxurieuse, et ses pieds ne peuvent se tenir au logis;
12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
car tantôt elle rode dehors, tantôt elle se tient à l'affût à tous les angles des places.
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
Puis elle l'arrête; elle l'embrasse, et lui dit d'une voix impudente
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
J'ai chez moi une victime pacifique; je rends grâce aujourd'hui;
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
c'est pour cela que je suis venue au-devant de toi; j'ai désiré ton visage, je t'ai trouvé.
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
J'ai tressé les sangles de mon lit, et l'ai couvert de doubles tapis d'Égypte.
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
J'ai parfumé ma couche de safran, et ma maison de cinnamome.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
Viens, et jouissons de l'amitié jusqu'à l'aurore; entre, et livrons-nous à l'amour.
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
Car mon mari n'est pas au logis; il est parti pour un long voyage.
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
Il a pris en sa main un grand sac d'argent; il ne reviendra pas de longtemps dans sa demeure.
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
Elle l'égare par ce flux de paroles; elle l'entraîne, avec le filet de ses lèvres.
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
Et lui la suit, sottement dupé, comme le bœuf se laisse conduire à la boucherie, et le chien à la chaîne,
23 mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
ou comme la biche frappée d'un trait au foie; il se hâte comme un oiseau attiré au piège, ne sachant pas qu'il court à la perte de son âme.
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
Maintenant donc, ô mon fils, écoute-moi, et sois attentif aux paroles de ma bouche.
25 Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
Garde-toi de laisser ton cœur s'égarer dans ses voies;
26 Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
car elle en a blessé et abattu beaucoup, et ceux qu'elle a tués sont innombrables.
27 Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )
Sa maison est le chemin de l'enfer, conduisant au réceptacle de la mort. (Sheol )