< Mithali 6 >
1 Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
O son my if you have stood surety for fellow-citizen your you have struck for the stranger palms your.
2 basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
You have been ensnared by [the] words of mouth your you have been caught by [the] words of mouth your.
3 Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
Do this then - O son my and deliver yourself for you have come in [the] palm of neighbor your go humble yourself and importune neighbor your.
4 Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
May not you give sleep to eyes your and slumber to eyelids your.
5 Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
Deliver yourself like a gazelle from a hand and like a bird from [the] hand of a fowler.
6 Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
Go to an ant O sluggard consider ways its and become wise.
7 Hana akida, afisa au mtawala,
Which not [belongs] to it [is] commander of icer and ruler.
8 lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
It prepares in the summer food its it gathers at the harvest food its.
9 Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
Until when? O sluggard - will you lie down when? will you rise from sleep your.
10 Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
A little of sleep a little of slumber a little of - folding of hands to rest.
11 ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
And it will come like a traveler poverty your and lack your like a man of shield.
12 Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
A person of worthlessness a person of wickedness [is] walking crookedness of mouth.
13 akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
[he is] winking (With eyes his *Q(K)*) [he is] scraping (with feet his *Q(K)*) [he is] pointing with fingers his.
14 Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
Perverse things - [are] in heart his [he is] devising evil at every time (contentions *Q(K)*) he sends out.
15 Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
There-fore suddenly it will come disaster his an instant he will be broken and there not [will be] healing.
16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
Six [things] those he hates Yahweh and [are] seven ([the] disgusting thing of *Q(K)*) self his.
17 Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
Eyes haughty a tongue of falsehood and hands [which] shed blood innocent.
18 moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
A heart [which] devises plans of wickedness feet [which] hurry to run to evil.
19 shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
[who] he breathes out Lies a witness of falsehood and [one who] spreads contentions between brothers.
20 Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Keep O son my [the] commandment of father your and may not you forsake [the] instruction of mother your.
21 Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
Bind them on heart your continually tie them on necks your.
22 utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
When walking about you - it will guide you when lying down you it will watch over you and you will awake it it will speak to you.
23 Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
For [is] a lamp [the] commandment and [the] instruction [is] a light and [are] a way of life rebukes of discipline.
24 Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
To keep you from a woman of evil from smoothness of tongue a foreign [woman].
25 Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
May not you desire beauty her in heart your and may not she capture you with eyelids her.
26 Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
For [the] price a woman a prostitute to a round loaf of bread and [the] wife of a man a life precious she hunts.
27 Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
¿ Will he snatch up a man fire in bosom his and garments his not will they be burned?
28 Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
Or? will he walk? a man on burning coals and feet his not will they be scorched.
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
[is] thus The [one who] goes into [the] wife of neighbor his not he will go unpunished every [one who] touches her.
30 Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
Not people despise the thief if he will steal to fill appetite his for he will be hungry.
31 Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
And he will be found out he will make restitution sevenfold all [the] wealth of house his he will give.
32 Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
[one who] commits adultery A woman [is] lacking of heart [one who] destroys own self his he he will do it.
33 Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
A wound and shame he will find and reproach his not it will be wiped away.
34 Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
For jealousy [is the] rage of a man and not he will have compassion on a day of vengeance.
35 Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.
Not he will lift up [the] face of any ransom and not he will be willing for you will make great a bribe.