< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
My son, if you be surety for your friend, if you have stricken your hand with a stranger,
2 basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
You are snared with the words of your mouth, you are taken with the words of your mouth.
3 Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
Do this now, my son, and deliver yourself, when you are come into the hand of your friend; go, humble yourself, and make sure your friend.
4 Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
Give not sleep to your eyes, nor slumber to your eyelids.
5 Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
Deliver yourself as a roe from the hand of the hunter, and as a bird from the hand of the fowler.
6 Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
Go to the ant, you sluggard; consider her ways, and be wise:
7 Hana akida, afisa au mtawala,
Which having no guide, overseer, or ruler,
8 lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
Provides her meat in the summer, and gathers her food in the harvest.
9 Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
How long will you sleep, O sluggard? when will you arise out of your sleep?
10 Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
Yet a little sleep, a little slumber, a little folding of the hands to sleep:
11 ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
So shall your poverty come as one that travels, and your want as an armed man.
12 Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
A naughty person, a wicked man, walks with a fraudulent mouth.
13 akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
He winks with his eyes, he speaks with his feet, he teaches with his fingers;
14 Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
Frowardness is in his heart, he devises mischief continually; he sows discord.
15 Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
Therefore shall his calamity come suddenly; suddenly shall he be broken without remedy.
16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
These six things does the LORD hate: yes, seven are an abomination to him:
17 Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
A proud look, a lying tongue, and hands that shed innocent blood,
18 moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
An heart that devises wicked imaginations, feet that be swift in running to mischief,
19 shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
A false witness that speaks lies, and he that sows discord among brothers.
20 Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
My son, keep your father’s commandment, and forsake not the law of your mother:
21 Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
Bind them continually on your heart, and tie them about your neck.
22 utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
When you go, it shall lead you; when you sleep, it shall keep you; and when you wake, it shall talk with you.
23 Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
For the commandment is a lamp; and the law is light; and reproofs of instruction are the way of life:
24 Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
To keep you from the evil woman, from the flattery of the tongue of a strange woman.
25 Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
Lust not after her beauty in your heart; neither let her take you with her eyelids.
26 Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
For by means of a whorish woman a man is brought to a piece of bread: and the adulteress will hunt for the precious life.
27 Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
Can a man take fire in his bosom, and his clothes not be burned?
28 Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
Can one go on hot coals, and his feet not be burned?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
So he that goes in to his neighbor’s wife; whoever touches her shall not be innocent.
30 Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
Men do not despise a thief, if he steal to satisfy his soul when he is hungry;
31 Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
But if he be found, he shall restore sevenfold; he shall give all the substance of his house.
32 Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
But whoever commits adultery with a woman lacks understanding: he that does it destroys his own soul.
33 Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
A wound and dishonor shall he get; and his reproach shall not be wiped away.
34 Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
For jealousy is the rage of a man: therefore he will not spare in the day of vengeance.
35 Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.
He will not regard any ransom; neither will he rest content, though you give many gifts.

< Mithali 6 >