< Mithali 5 >

1 Mwanangu, zingatia hekima yangu; sikiliza kwa makini ufahamu wangu,
我儿,要留心我智慧的话语, 侧耳听我聪明的言词,
2 ili ujifunze busara na midomo yako iweze kuhifadhi maarifa.
为要使你谨守谋略, 嘴唇保存知识。
3 Maana midomo ya malaya hutiririsha asali na kinywa chake ni laini kuliko mafuta,
因为淫妇的嘴滴下蜂蜜; 她的口比油更滑,
4 lakini mwishoni anakuwa mchungu kama mnyoo, hukata kama upunga mkali.
至终却苦似茵 , 快如两刃的刀。
5 Miguu yake huelekea mauti; hatua zake huelekea njia yote ya kuzimu. (Sheol h7585)
她的脚下入死地; 她脚步踏住阴间, (Sheol h7585)
6 Hafikirii njia ya uzima. Hatua za miguu yake hupotea, maana hajui anakwenda wapi.
以致她找不着生命平坦的道。 她的路变迁不定, 自己还不知道。
7 Sasa, wanangu, nisikilizeni; wala msiache kusikiliza maneno ya kinywa changu.
众子啊,现在要听从我; 不可离弃我口中的话。
8 Lindeni njia yenu mbali naye wala msiende karibu na mlango wa nyumba yake.
你所行的道要离她远, 不可就近她的房门,
9 Kwa njia hiyo hamtawapa wengine heshima yenu au miaka ya uzima wenu kwa mtu mkatiri;
恐怕将你的尊荣给别人, 将你的岁月给残忍的人;
10 wageni usije kufanya karamu kwa utajiri wenu; kazi mliyoifanya haitaenda katika nyumba ya wageni.
恐怕外人满得你的力量, 你劳碌得来的,归入外人的家;
11 Mwishoni mwa maisha yenu mtajuta ambapo nyama na mwili wenu vitaangamia.
终久,你皮肉和身体消毁, 你就悲叹,
12 Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
说:我怎么恨恶训诲, 心中藐视责备,
13 Sikuweza kuwatii walimu wangu au kuwasikiliza walionielekeza.
也不听从我师傅的话, 又不侧耳听那教训我的人?
14 Nilikuwa nimeharibika kabisa katikati ya kusanyiko, miongoni mwa makutano ya watu.”
我在圣会里, 几乎落在诸般恶中。
15 Munywe maji kutoka kwenye birika lenu mwenyewe na munywe maji yanatiririka kutoka kwenye kisima chenu.
你要喝自己池中的水, 饮自己井里的活水。
16 Je inapaswa chemichemi yenu ifurike popote na mifereji yenu ya maji itiririke katika njia kuu?
你的泉源岂可涨溢在外? 你的河水岂可流在街上?
17 Yawe yenu wenyewe peke yenu wala si kwa wageni.
惟独归你一人, 不可与外人同用。
18 Chemichemi yako ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
要使你的泉源蒙福; 要喜悦你幼年所娶的妻。
19 Maana ni ayala apendezaye na kulungu mwenye uzuri. Matiti yake na yakujaze furaha muda wote; daima na utekwe na upendo wake.
她如可爱的麀鹿,可喜的母鹿; 愿她的胸怀使你时时知足, 她的爱情使你常常恋慕。
20 Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
我儿,你为何恋慕淫妇? 为何抱外女的胸怀?
21 Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
因为,人所行的道都在耶和华眼前; 他也修平人一切的路。
22 Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
恶人必被自己的罪孽捉住; 他必被自己的罪恶如绳索缠绕。
23 Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.
他因不受训诲就必死亡; 又因愚昧过甚,必走差了路。

< Mithali 5 >