< Mithali 4 >
1 Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
Oíd hijos la enseñanza del padre; y estád atentos, para que sepáis inteligencia.
2 Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
Porque os doy buen enseñamiento: no desamparéis mi ley.
3 Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
Porque yo fui hijo de mi padre, delicado y único delante de mi madre:
4 baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
Y enseñábame, y me decía: Sustente mis razones tu corazón: guarda mis mandamientos, y vivirás.
5 Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
Adquiere sabiduría, adquiere inteligencia: no te olvides, ni te apartes de las razones de mi boca.
6 usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
No la dejes, y ella te guardará; ámala, y conservarte ha.
7 Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
Primeramente sabiduría: adquiere sabiduría, y ante toda tu posesión adquiere inteligencia.
8 Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
Engrandécela, y ella te engrandecerá; ella te honrará, cuando tú la hubieres abrazado.
9 Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
Dará a tu cabeza aumento de gracia: corona de hermosura te entregará.
10 Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
Oye, hijo mío, y recibe mis razones; y multiplicársete han años de vida.
11 Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
Por el camino de la sabiduría te he encaminado; y por veredas derechas te he hecho andar.
12 Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
Cuando por ellas anduvieres, no se estrecharán tus pasos; y si corrieres, no tropezarás.
13 Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
Ten asida la instrucción, no la dejes: guárdala, porque ella es tu vida.
14 Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
No entres por la vereda de los impíos: ni vayas por el camino de los malos:
15 Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
Desampárala; no pases por ella: apártate de ella, y pasa.
16 Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
Porque no duermen, si no hicieren mal; y pierden su sueño, si no han hecho caer.
17 Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
Porque comen pan de maldad, y beben vino de robos.
18 Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
Mas la vereda de los justos es como la luz del lucero: auméntase, y alumbra hasta que el día es perfecto.
19 Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
El camino de los impíos es como la oscuridad: no saben en qué tropiezan.
20 Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
Hijo mío, está atento a mis palabras; y a mis razones inclina tu oreja:
21 Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
No se aparten de tus ojos: mas guárdalas en medio de tu corazón;
22 Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
Porque son vida a los que las hallan; y medicina a toda su carne.
23 Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
Sobre toda cosa guardada, guarda tu corazón; porque de él mana la vida.
24 Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.
Aparta de ti la perversidad de la boca; y la iniquidad de labios aleja de ti.
25 Macho yako yatazame mbele kwa unyoofu na kwa uthabiti tazama mbele sawasawa.
Tus ojos miren lo recto; y tus párpados enderecen tu camino delante de ti.
26 Usawazishe pito la mguu wako; na njia zako zote zitakuwa salama.
Pesa la vereda de tus pies; y todos tus caminos sean ordenados.
27 Usigeuke upande wa kulia au kushoto; ondoa mguu wako mbali na uovu.
No te apartes a diestra, ni a siniestra: aparta tu pie del mal.