< Mithali 31 >
1 Maneno ya mfalme Lemueli - mausia aliyofundishwa na mama yake.
PALABRAS del rey Lemuel; la profecía con que le enseñó su madre.
2 Mwanangu nini? Na ni nini mwana wa tumbo langu? Na ni nini mwana wa nadhiri zangu?
¿Qué, hijo mío? ¿y qué, hijo de mi vientre? ¿y qué, hijo de mis deseos?
3 Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
No des á las mujeres tu fuerza, ni tus caminos á lo que es para destruir los reyes.
4 Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
No es de los reyes, oh Lemuel, no es de los reyes beber vino, ni de los príncipes la cerveza.
5 Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
No sea que bebiendo olviden la ley, y perviertan el derecho de todos los hijos afligidos.
6 Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
Dad la cerveza al desfallecido, y el vino á los de amargo ánimo:
7 Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
Beban, y olvídense de su necesidad, y de su miseria no más se acuerden.
8 Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
Abre tu boca por el mudo, en el juicio de todos los hijos de muerte.
9 Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
Abre tu boca, juzga justicia, y el derecho del pobre y del menesteroso.
10 Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
Mujer fuerte, ¿quién la hallará? porque su estima sobrepuja largamente á [la de] piedras preciosas.
11 Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
El corazón de su marido está en ella confiado, y no tendrá necesidad de despojo.
12 Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
Darále ella bien y no mal, todos los días de su vida.
13 Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
Buscó lana y lino, y con voluntad labró de sus manos.
14 Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
Fué como navío de mercader: trae su pan de lejos.
15 Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
Levantóse aun de noche, y dió comida á su familia, y ración á sus criadas.
16 Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
Consideró la heredad, y compróla; y plantó viña del fruto de sus manos.
17 Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
Ciñó sus lomos de fortaleza, y esforzó sus brazos.
18 Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
Gustó que era buena su granjería: su candela no se apagó de noche.
19 Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
Aplicó sus manos al huso, y sus manos tomaron la rueca.
20 Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
Alargó su mano al pobre, y extendió sus manos al menesteroso.
21 Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
No tendrá temor de la nieve por su familia, porque toda su familia está vestida de ropas dobles.
22 Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
Ella se hizo tapices; de lino fino y púrpura es su vestido.
23 Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
Conocido es su marido en las puertas, cuando se sienta con los ancianos de la tierra.
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
Hizo telas, y vendió; y dió cintas al mercader.
25 Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
Fortaleza y honor son su vestidura; y en el día postrero reirá.
26 Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
Abrió su boca con sabiduría: y la ley de clemencia está en su lengua.
27 Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
Considera los caminos de su casa, y no come el pan de balde.
28 Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
Levantáronse sus hijos, y llamáronla bienaventurada; y su marido también la alabó.
29 “Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
Muchas mujeres hicieron el bien; mas tú las sobrepujaste á todas.
30 Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
Engañosa es la gracia, y vana la hermosura: la mujer que teme á Jehová, ésa será alabada.
31 Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.
Dadle el fruto de sus manos, y alábenla en las puertas sus hechos.