< Mithali 31 >

1 Maneno ya mfalme Lemueli - mausia aliyofundishwa na mama yake.
דברי למואל מלך משא אשר יסרתו אמו׃
2 Mwanangu nini? Na ni nini mwana wa tumbo langu? Na ni nini mwana wa nadhiri zangu?
מה ברי ומה בר בטני ומה בר נדרי׃
3 Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
אל תתן לנשים חילך ודרכיך למחות מלכין׃
4 Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
אל למלכים למואל אל למלכים שתו יין ולרוזנים או שכר׃
5 Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
פן ישתה וישכח מחקק וישנה דין כל בני עני׃
6 Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
תנו שכר לאובד ויין למרי נפש׃
7 Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
ישתה וישכח רישו ועמלו לא יזכר עוד׃
8 Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
פתח פיך לאלם אל דין כל בני חלוף׃
9 Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
פתח פיך שפט צדק ודין עני ואביון׃
10 Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
אשת חיל מי ימצא ורחק מפנינים מכרה׃
11 Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
בטח בה לב בעלה ושלל לא יחסר׃
12 Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
גמלתהו טוב ולא רע כל ימי חייה׃
13 Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
דרשה צמר ופשתים ותעש בחפץ כפיה׃
14 Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
היתה כאניות סוחר ממרחק תביא לחמה׃
15 Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
ותקם בעוד לילה ותתן טרף לביתה וחק לנערתיה׃
16 Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
זממה שדה ותקחהו מפרי כפיה נטע כרם׃
17 Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
חגרה בעוז מתניה ותאמץ זרעותיה׃
18 Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
טעמה כי טוב סחרה לא יכבה בליל נרה׃
19 Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
ידיה שלחה בכישור וכפיה תמכו פלך׃
20 Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
כפה פרשה לעני וידיה שלחה לאביון׃
21 Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
לא תירא לביתה משלג כי כל ביתה לבש שנים׃
22 Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
מרבדים עשתה לה שש וארגמן לבושה׃
23 Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
נודע בשערים בעלה בשבתו עם זקני ארץ׃
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
סדין עשתה ותמכר וחגור נתנה לכנעני׃
25 Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
עז והדר לבושה ותשחק ליום אחרון׃
26 Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
פיה פתחה בחכמה ותורת חסד על לשונה׃
27 Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
צופיה הליכות ביתה ולחם עצלות לא תאכל׃
28 Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
קמו בניה ויאשרוה בעלה ויהללה׃
29 “Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
רבות בנות עשו חיל ואת עלית על כלנה׃
30 Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
שקר החן והבל היפי אשה יראת יהוה היא תתהלל׃
31 Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.
תנו לה מפרי ידיה ויהללוה בשערים מעשיה׃

< Mithali 31 >