< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
しばしばしかられても、なおかたくなな者は、たちまち打ち敗られて助かることはない。
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
正しい者が権力を得れば民は喜び、悪しき者が治めるとき、民はうめき苦しむ。
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
知恵を愛する人はその父を喜ばせ、遊女に交わる者はその資産を浪費する。
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
王は公儀をもって国を堅くする、しかし、重税を取り立てる者はこれを滅ぼす。
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
その隣り人にへつらう者は、彼の足の前に網を張る。
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
悪人は自分の罪のわなに陥る、しかし正しい人は喜び楽しむ。
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
正しい人は貧しい者の訴えをかえりみる、悪しき人はそれを知ろうとはしない。
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
あざける人は町を乱し、知恵ある者は怒りを静める。
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
知恵ある人が愚かな人と争うと、愚かな者はただ怒り、あるいは笑って、休むことがない。
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
血に飢えている人は罪のない者を憎む、悪しき者は彼の命を求める。
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
愚かな者は怒りをことごとく表わし、知恵ある者は静かにこれをおさえる。
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
もし治める者が偽りの言葉に聞くならば、その役人らはみな悪くなる。
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
貧しい者と、しえたげる者とは共に世におる、主は彼ら両者の目に光を与えられる。
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
もし王が貧しい者を公平にさばくならば、その位はいつまでも堅く立つ。
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
むちと戒めとは知恵を与える、わがままにさせた子はその母に恥をもたらす。
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
悪しき者が権力を得ると罪も増す、正しい者は彼らの倒れるのを見る。
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
あなたの子を懲しめよ、そうすれば彼はあなたを安らかにし、またあなたの心に喜びを与える。
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
預言がなければ民はわがままにふるまう、しかし律法を守る者はさいわいである。
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
しもべは言葉だけで訓練することはできない、彼は聞いて知っても、心にとめないからである。
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
言葉の軽率な人を見るか、彼よりもかえって愚かな者のほうに望みがある。
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
しもべをその幼い時からわがままに育てる人は、ついにはそれを自分のあとつぎにする。
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
怒る人は争いを起し、憤る人は多くの罪を犯す。
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
人の高ぶりはその人を低くし、心にへりくだる者は誉を得る。
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
盗びとにくみする者は自分の魂を憎む、彼はのろいを聞いても何事をも口外しない。
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
人を恐れると、わなに陥る、主に信頼する者は安らかである。
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
治める者の歓心を得ようとする人は多い、しかし人の事を定めるのは主による。
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
正しい人は不正を行う人を憎み、悪しき者は正しく歩む人を憎む。

< Mithali 29 >