< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
L'uomo che, rimproverato, resta di dura cervice sarà spezzato all'improvviso e senza rimedio.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
Quando comandano i giusti, il popolo gioisce, quando governano gli empi, il popolo geme.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
Chi ama la sapienza allieta il padre, ma chi frequenta prostitute dissipa il patrimonio.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
Il re con la giustizia rende prospero il paese, l'uomo che fa esazioni eccessive lo rovina.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
L'uomo che adula il suo prossimo gli tende una rete per i suoi passi.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
Sotto i passi del malvagio c'è un trabocchetto, mentre il giusto corre ed è contento.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
Il giusto si prende a cuore la causa dei miseri, ma l'empio non intende ragione.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
I beffardi mettono sottosopra una città, mentre i saggi placano la collera.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
Se un saggio discute con uno stolto, si agiti o rida, non vi sarà conclusione.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Gli uomini sanguinari odiano l'onesto, mentre i giusti hanno cura di lui.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
Lo stolto dà sfogo a tutto il suo malanimo, il saggio alla fine lo sa calmare.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
Se un principe dà ascolto alle menzogne, tutti i suoi ministri sono malvagi.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
Il povero e l'usuraio si incontrano; è il Signore che illumina gli occhi di tutti e due.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
Un re che giudichi i poveri con equità rende saldo il suo trono per sempre.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
La verga e la correzione danno sapienza, ma il giovane lasciato a se stesso disonora sua madre.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
Quando governano i malvagi, i delitti abbondano, ma i giusti ne vedranno la rovina.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Correggi il figlio e ti farà contento e ti procurerà consolazioni.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
Senza la rivelazione il popolo diventa sfrenato; beato chi osserva la legge.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
Lo schiavo non si corregge a parole, comprende, infatti, ma non obbedisce.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Hai visto un uomo precipitoso nel parlare? C'è più da sperare in uno stolto che in lui.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
Chi accarezza lo schiavo fin dall'infanzia, alla fine costui diventerà insolente.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
Un uomo collerico suscita litigi e l'iracondo commette molte colpe.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
L'orgoglio dell'uomo ne provoca l'umiliazione, l'umile di cuore ottiene onori.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
Chi è complice del ladro, odia se stesso, egli sente l'imprecazione, ma non denuncia nulla.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
Il temere gli uomini pone in una trappola; ma chi confida nel Signore è al sicuro.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Molti ricercano il favore del principe, ma è il Signore che giudica ognuno.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
L'iniquo è un abominio per i giusti e gli uomini retti sono in abominio ai malvagi.

< Mithali 29 >