< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
איש תוכחות מקשה-ערף-- פתע ישבר ואין מרפא
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
ברבות צדיקים ישמח העם ובמשל רשע יאנח עם
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
איש-אהב חכמה ישמח אביו ורעה זונות יאבד-הון
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
מלך--במשפט יעמיד ארץ ואיש תרומות יהרסנה
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
גבר מחליק על-רעהו רשת פורש על-פעמיו
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
בפשע איש רע מוקש וצדיק ירון ושמח
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
ידע צדיק דין דלים רשע לא-יבין דעת
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
אנשי לצון יפיחו קריה וחכמים ישיבו אף
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
איש-חכם--נשפט את-איש אויל ורגז ושחק ואין נחת
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
אנשי דמים ישנאו-תם וישרים יבקשו נפשו
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
כל-רוחו יוציא כסיל וחכם באחור ישבחנה
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
משל מקשיב על-דבר-שקר-- כל-משרתיו רשעים
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
רש ואיש תככים נפגשו-- מאיר עיני שניהם יהוה
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
מלך שופט באמת דלים-- כסאו לעד יכון
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
שבט ותוכחת יתן חכמה ונער משלח מביש אמו
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
ברבות רשעים ירבה-פשע וצדיקים במפלתם יראו
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
יסר בנך ויניחך ויתן מעדנים לנפשך
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
באין חזון יפרע עם ושמר תורה אשרהו
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
בדברים לא-יוסר עבד כי-יבין ואין מענה
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
חזית--איש אץ בדבריו תקוה לכסיל ממנו
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
מפנק מנער עבדו ואחריתו יהיה מנון
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
איש-אף יגרה מדון ובעל חמה רב-פשע
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
גאות אדם תשפילנו ושפל-רוח יתמך כבוד
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
חולק עם-גנב שונא נפשו אלה ישמע ולא יגיד
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
חרדת אדם יתן מוקש ובוטח ביהוה ישגב
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
רבים מבקשים פני-מושל ומיהוה משפט-איש
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
תועבת צדיקים איש עול ותועבת רשע ישר-דרך

< Mithali 29 >