< Mithali 29 >
1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
He that being often reproved stiffeneth his neck, suddenly shall be hurt, and there be no healing.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
When the righteous become great, the people rejoice, but, when a lawless man beareth rule, a people sigh.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
A man who loveth wisdom, gladdeneth his father, but, a companion of harlots, destroyeth wealth.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
A king, by justice, shall establish a land, —but, a man open to bribes, bringeth it to ruin.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
A man who flattereth his neighbour, spreadeth, a net, over his steps.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
In the transgression of a wicked man, is a snare, but, the righteous, doth shout in triumph and rejoice.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
The righteous doth acknowledge the plea of the poor, but, the lawless, regardeth not knowledge.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Men given to mockery, inflame a city, —but, wise men, turn away anger.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
A wise man pleading with a foolish man, whether he rage or laugh, there is no settlement.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Blood-thirsty men, hate the blameless man, and, as for the upright, they seek his life.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
All his anger, doth a dullard let go, but, a wise man, by keeping it back, stilleth it.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
When a ruler giveth heed to the word of falsehood, all his attendants, become lawless.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
The poor man and the man of usury, meet together, he that enlighteneth the eyes of them both, is Yahweh.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
When a king judgeth faithfully the poor, his throne, to futurity, shall be established.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
A rod with rebuke, giveth wisdom, but, a youth unrestrained, bringeth shame to his mother.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
When the lawless become great, transgression increaseth, but, the righteous, shall behold, their ruin.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Correct thy son, that he may give thee rest, that he may give delight to thy soul.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
Where there is no vision, a people is let loose, but, he that keepeth instruction, how happy is he!
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
By words, a servant will not be corrected, though he perceiveth, yet is there no answer.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Thou hast seen a man hasty in his words, —there is, more hope of a dullard, than of him.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
He that dealeth tenderly with his servant from childhood, in his after life, shall have him for a son.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
A man given to anger, stirreth up strife, and, he that exceedeth in wrath, aboundeth in transgression.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
The loftiness of a man, layeth him low, —but, one of a lowly spirit, shall attain unto honour.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
He that shareth with a thief, hateth himself, an oath, he heareth, yet may not tell.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
The fear of man, setteth a snare, but, he that trusteth in Yahweh, shall be placed on high.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Many, seek the face of a ruler, but, from Yahweh, is the sentence of each one.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
An abomination to the righteous, is the man of perversity, and, an abomination to the lawless, is a man of straightforward way.