< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
He who, being often reproved, hardeneth his neck, Shall suddenly be destroyed, and that without remedy.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
When the righteous are powerful, the people rejoice; But when the wicked beareth rule, the people mourn.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
He who loveth wisdom rejoiceth his father; But he who is a companion of harlots destroyeth his substance.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
A king by equity establisheth a land; But he who receiveth gifts overthroweth it.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
A man who flattereth his neighbor Spreadeth a net for his feet.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
In the transgression of a wicked man there is a snare; But the righteous shall sing and rejoice.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
A righteous man careth for the cause of the poor; A wicked man discerneth not knowledge.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Scoffers kindle a city into a flame; But wise men pacify wrath.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
If a wise man contend in a cause with a fool, Whether he rage or laugh, there will be no rest.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
The bloodthirsty man hateth the upright; But the righteous seek to preserve his life.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
A fool letteth all his anger come out; But a wise man keepeth it back.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
If a ruler listen to words of falsehood, All his servants become wicked.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
The poor man and the oppressor meet together: The LORD giveth light to the eyes of them both.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
The king that judgeth the poor with uprightness, His throne shall be established for ever.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
The rod and reproof give wisdom; But a child left to himself bringeth shame to his mother.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
When the wicked are powerful, transgression increaseth; But the righteous shall see their fall.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Chastise thy son, and he will give thee rest; Yea, he will give delight to thy soul.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
Where there is no vision, the people become unruly; But he that keepeth the law, happy is he.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
A servant will not be corrected by words; For, though he understand, he will not obey.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Seest thou a man hasty in his words? There is more hope of a fool than of him.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
He that bringeth up his servant delicately from childhood Shall have him become a son at the last.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
An angry man stirreth up strife, And a passionate man aboundeth in transgression.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
A man's pride will bring him low; But he that is of a humble spirit shall obtain honor.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
He who shareth with a thief hateth himself: He heareth the curse, but maketh no discovery.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
The fear of man bringeth a snare; But whoso putteth his trust in the LORD shall be safe.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Many are they who seek the ruler's favor; But every man's judgment cometh from the LORD.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
As the unjust man is an abomination to the righteous, So the upright in his way is an abomination to the wicked.

< Mithali 29 >