< Mithali 29 >
1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
A reprover is better than a stiff-necked man: for when the latter is suddenly set on fire, there shall be no remedy.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
When the righteous are praised, the people will rejoice: but when the ungodly rule, men mourn.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
When a man loves wisdom, his father rejoices: but he that keeps harlots will waste wealth.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
A righteous king establishes a country: but a transgressor destroys [it].
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
He that prepares a net in the way of his own friend, entangles his own feet in it.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
A great snare [is spread] for a sinner: but the righteous shall be in joy and gladness.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
A righteous man knows how to judge for the poor: but the ungodly understands not knowledge; and the poor man has not an understanding mind.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Lawless men burn down a city: but wise men turn away wrath.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
A wise man shall judge nations: but a worthless man being angry laughs and fears not.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Bloody men hate a holy [person], but the upright will seek his soul.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
A fool utters all is mind: but the wise reserves his in part.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
When a king hearkens to unjust language, all his subjects are transgressors.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
When the creditor and debtor meet together, the Lord oversees them both.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
When a king judges the poor in truth, his throne shall be established for a testimony.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
Stripes and reproofs give wisdom: but an erring child disgraces his parents.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
When the ungodly abound, sins abound: but when they fall, the righteous are warned.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Chasten your son, and he shall give you rest; and he shall give honor to your soul.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
There shall be no interpreter to a sinful nation: but he that observes the law is blessed.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
A stubborn servant will not be reproved by words: for even if he understands, still he will not obey.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
If you see a man hasty in [his] words, know that the fool has hope rather than he.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
He that lives wantonly from a child, shall be a servant, and in the end shall grieve over himself.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
A furious man stirs up strife, and a passionate man digs up sin.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
Pride brings a man low, but the Lord upholds the humble-minded with honor.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
He that shares with a thief, hates his own soul: and if any having heard an oath uttered tell not of it,
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
[they] fearing and reverencing men [unreasonably] have been overthrown, but he that trusts in the Lord shall rejoice. Ungodliness causes a man to stumble: but he that trusts in his master shall be safe.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Many wait on the favor of rulers; but justice comes to a man from the Lord.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
A righteous man is an abomination to an unrighteous man, and the direct way is an abomination to the sinner.