< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
The man who, with a stiff neck, treats the one who corrects him with contempt will be suddenly overwhelmed to his own destruction, and reason shall not follow him.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
When just men are multiplied, the common people shall rejoice. When the impious take up the leadership, the people shall mourn.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
The man who loves wisdom rejoices his father. But whoever nurtures promiscuous women will lose his substance.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
A just king guides the land. A man of avarice will destroy it.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
A man who speaks to his friend with flattering and feigned words spreads a net for his own feet.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
A snare will entangle the iniquitous when he sins. And the just shall praise and be glad.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
The just knows the case of the poor. The impious is ignorant of knowledge.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Pestilent men squander a city. Yet truly, the wise avert fury.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
A wise man, if he were to contend with the foolish, whether in anger or in laughter, would find no rest.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Bloodthirsty men hate the simple one; but the just seek out his soul.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
A foolish one offers everything on his mind. A wise one reserves and defers until later.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
A leader who freely listens to lying words has only impious servants.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
The pauper and the creditor have met one another. The Lord is the illuminator of them both.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
The king who judges the poor in truth, his throne shall be secured in eternity.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
The rod and its correction distribute wisdom. But the child who is left to his own will, brings shame to his mother.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
When the impious are multiplied, crimes will be multiplied. But the just shall see their ruin.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Teach your son, and he will refresh you, and he will give delight to your soul.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
When prophecy fails, the people will be scattered. Yet truly, whoever guards the law is blessed.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
A servant cannot be taught by words, because he understands what you say, but he disdains to respond.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Have you seen a man rushing to speak? Foolishness has more hope than his correction.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
Whoever nurtures his servant delicately from childhood, afterwards will find him defiant.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
A short-tempered man provokes quarrels. And whoever is easily angered is more likely to sin.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
Humiliation follows the arrogant. And glory shall uphold the humble in spirit.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
Whoever participates with a thief hates his own soul; for he listens to his oath and does not denounce him.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
Whoever fears man will quickly fall. Whoever hopes in the Lord shall be lifted up.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Many demand the face of the leader. But the judgment of each one proceeds from the Lord.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
The just abhor an impious man. And the impious abhor those who are on the right way. By keeping the word, the son shall be free from perdition.

< Mithali 29 >