< Mithali 28 >
1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
Los malvados huyen cuando nadie los persigue; pero los justos son audaces como un león.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
En la rebelión, una tierra tiene muchos gobernantes, pero el orden es mantenido por un hombre de entendimiento y conocimiento.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
Un necesitado que oprime a los pobres es como una lluvia torrencial que no deja cosechas.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Los que abandonan la ley alaban a los malvados; pero los que guardan la ley se enfrentan a ellos.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Los hombres malvados no entienden la justicia; pero los que buscan a Yahvé lo comprenden plenamente.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Mejor es el pobre que camina en su integridad que el que es perverso en sus caminos, y es rico.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
El que guarda la ley es un hijo sabio; pero el que es compañero de los glotones avergüenza a su padre.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
El que aumenta su riqueza con intereses excesivos lo recoge para quien se apiada de los pobres.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
El que aparta su oído para no oír la ley, incluso su oración es una abominación.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
El que hace que los rectos se extravíen por el mal camino, caerá en su propia trampa; pero los irreprochables heredarán el bien.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
El rico es sabio a sus propios ojos; pero el pobre que tiene entendimiento ve a través de él.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
Cuando los justos triunfan, hay gran gloria; pero cuando los malvados se levantan, los hombres se esconden.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
El que oculta sus pecados no prospera, pero quien se confiesa y renuncia a ellos encuentra la misericordia.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Dichoso el hombre que siempre teme; pero el que endurece su corazón cae en el problema.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
Como un león que ruge o un oso que embiste, así es un gobernante malvado sobre gente indefensa.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
Un gobernante tirano carece de juicio. Quien odia la ganancia mal habida tendrá días largos.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
El hombre atormentado por la culpa de la sangre será un fugitivo hasta la muerte. Nadie lo apoyará.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
Quien camina sin culpa se mantiene a salvo; pero uno con caminos perversos caerá de repente.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
El que trabaja su tierra tendrá abundancia de alimentos; pero el que persigue fantasías se saciará de pobreza.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
Un hombre fiel es rico en bendiciones; pero el que está ansioso por ser rico no quedará impune.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
Mostrar parcialidad no es bueno, pero un hombre hará el mal por un pedazo de pan.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
El hombre tacaño se apresura a buscar las riquezas, y no sabe que la pobreza le espera.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
El que reprende a un hombre encontrará después más favor que el que adula con la lengua.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
El que roba a su padre o a su madre y dice: “No está mal”. es un socio con un destructor.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
El que es codicioso suscita conflictos; pero el que confía en Yahvé prosperará.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
El que confía en sí mismo es un necio; pero el que camina en la sabiduría se mantiene a salvo.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
Al que da a los pobres no le falta nada; pero el que cierra los ojos tendrá muchas maldiciones.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Cuando los malvados se levantan, los hombres se esconden; pero cuando perecen, los justos prosperan.