< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
Les méchants fuient sans qu’on les poursuive, mais les justes ont de l’assurance comme un lion.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
Dans un pays en révolte, les chefs se multiplient; mais avec un homme intelligent et sage l’ordre se prolonge.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
Un homme pauvre qui opprime les malheureux, c’est une pluie violente qui cause la disette.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Ceux qui abandonnent la loi louent le méchant, ceux qui l’observent s’irritent contre lui.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Les hommes pervers ne comprennent pas ce qui est juste, mais ceux qui cherchent Yahweh comprennent tout.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Mieux vaut le pauvre dans son intégrité que l’homme aux voies tortueuses et qui est riche.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
Celui qui observe la loi est un fils intelligent, mais celui qui nourrit les débauchés fait honte à son père.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
Celui qui augmente ses biens par l’intérêt et l’usure les amasse pour celui qui a pitié des pauvres.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Si quelqu’un détourne l’oreille pour ne pas écouter la loi, sa prière même est une abomination.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
Celui qui égare les hommes droits dans la voie mauvaise tombera lui-même dans la fosse qu’il a creusée; mais les hommes intègres posséderont le bonheur.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
L’homme riche est sage à ses yeux; mais le pauvre intelligent le connaît.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
Quand les justes triomphent, c’est une grande fête; quand les méchants se lèvent, chacun se cache.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
Celui qui cache ses fautes ne prospérera point, mais celui qui les avoue et les quitte obtiendra miséricorde.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Heureux l’homme qui est continuellement dans la crainte! Mais celui qui endurcit son cœur tombera dans le malheur.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
Un lion rugissant et un ours affamé, tel est le méchant qui domine sur un peuple pauvre.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
Le prince sans intelligence multiplie l’oppression, mais celui qui hait la cupidité aura de longs jours.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
Un homme chargé du sang d’un autre fuit jusqu’à la fosse: ne l’arrêtez pas!
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
Celui qui marche dans l’intégrité trouvera le salut, mais celui qui suit des voies tortueuses tombera pour ne plus se relever.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
Celui qui cultive son champ sera rassasié de pain, mais celui qui poursuit des choses vaines sera rassasié de pauvreté.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
Un homme fidèle sera comblé de bénédictions, mais celui qui a hâte de s’enrichir n’échappera pas à la faute.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
Il n’est pas bon de faire acception des personnes; pour un morceau de pain un homme devient criminel.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
L’homme envieux a hâte de s’enrichir; il ne sait pas que la disette viendra sur lui.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
Celui qui reprend quelqu’un trouve ensuite plus de faveur que celui qui rend sa langue flatteuse.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
Celui qui vole son père et sa mère, et qui dit: « Ce n’est pas un péché, » c’est le compagnon du brigand.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
L’homme cupide excite les querelles; mais celui qui se confie en Yahweh sera rassasié.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
Celui qui a confiance dans son propre cœur est un insensé, mais celui qui marche dans la sagesse sera sauvé.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
Celui qui donne au pauvre n’éprouve pas la disette, mais celui qui ferme les yeux est chargé de malédictions.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Quand les méchants s’élèvent, chacun se cache; quand ils périssent, les justes se multiplient.

< Mithali 28 >