< Mithali 28 >
1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
They flee and there not [is one who] pursues [the] wicked and righteous [people] like a young lion he is confident.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
By [the] transgression of a land [are] many princes its and by a person understanding knowing thus it will last long.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
A man poor and [who] oppresses poor [people] rain [which] washes away and there not [is] food.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
[those who] forsake [the] law They praise [the] wicked and [those who] keep [the] law they engage in strife with them.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
People of evil not they understand justice and [those who] seek Yahweh they understand everything.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
[is] good A poor [person] [who] walks in integrity his more than [the] [person] perverse of two ways and he [is] rich.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
[one who] keeps [the] law [is] a son Understanding and [one who] associates with gluttons he shames father his.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
[one who] increases Wealth his by interest (and usury *Q(K)*) for [one who] shows favor to poor [people] he gathers it.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
[one who] turns aside Ear his from hearing [the] law also prayer his [is] an abomination.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
[one who] leads astray Upright [people] - in a way evil in own pit his he he will fall and blameless [people] they will inherit good.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
[is] wise In own eyes his a person rich and a poor [person] understanding he examines thoroughly him.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
When rejoice righteous [people] great glory and when arise wicked [people] he is searched for everyone.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
[one who] conceals Transgressions his not he will prosper and [one who] confesses and [one who] forsakes [them] he will be shown mercy.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
How blessed! [is] a person [who] fears continually and [one who] hardens heart his he will fall in calamity.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
A lion roaring and a bear rushing a ruler wicked over a people poor.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
A ruler lacking of understanding and great of extortion ([one who] hates *Q(K)*) unjust gain he will prolong days.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
A person oppressed by [the] blood of a life to [the] pit he will flee may not people support him.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
[one who] walks Blameless he will be delivered and [one who] is crooked of two ways he will fall at one.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
[one who] tills Land his he will be satisfied food and [one who] pursues empty [things] he will be satisfied poverty.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
A person of faithfulness [will be] great of blessings and [one who] hastens to gain riches not he will go unpunished.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
To pay regard to face not [is] good and on a piece of bread he will transgress a man.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
[is] hastening To wealth a person evil of eye and not he knows that poverty it will come to him.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
[one who] reproves A person after me favor he will find more than [one who] makes smooth [the] tongue.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
[one who] robs - Father his and mother his and [one who] says there not [is] a transgression [is] a companion he of a person of destruction.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
A [person] arrogant of self he stirs up strife and [one who] relies on Yahweh he will be made fat.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
[one who] trusts In own heart his he [is] a fool and [one who] walks in wisdom he he will be delivered.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
[one who] gives To the poor there not [is] lack and [one who] hides eyes his great of curses.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
When arise wicked [people] he hides himself everyone and when perish they they increase righteous [people].